Kibondo; Shule za sekondari zilizoko vijijini hapa nchini zinakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwaemo ukosefu wa umememe wa uhakika kwa ajili ya kuendeshea maabara licha ya serikali kutilia mkazo ujenzi wa maabara hatua inayoweza kukwamisha ndoto za wanafunzi hasa wa masomo ya sayansiWahitimu wa kidato cha sita Shule ya sekondari wasichana Bon Consilii

Wahitimu wa kidato cha sita shule ya sekondari wasichana Bon concilii Mabamba



Dr Ibrahim Mgeni rasmi



Janeroza Mpilirwe mkuu wa shule Bon consilii
Kibondo; Shule za sekondari zilizoko vijijini hapa nchini zinakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwaemo ukosefu wa umememe wa uhakika  kwa ajili ya kuendeshea maabara licha ya serikali kutilia mkazo ujenzi wa maabara  hatua inayoweza kukwamisha ndoto za wanafunzi hasa wa masomo ya sayansi

Wakizungumza  juzi wanafunzi wa shule ya sekondari ya wasichana  Bon consilii iliyoko wilayani Kibondo mkoani kigoma katika mahafali ya 12 ya kuhitimu Kidato cha sita ambao ni Isabela Kilongozi na Irene Masabo walisema kuwa ukosefu wa umeme wa uhakika kwa shule zilizoko vijijini  hawapati fulsa nzuri ya kujifunza hasa masomo ya sayansi kwakuwa maabara hizo lazima  zitegeme umeme

Aidha  walisema tatizo la uhaba wa walimu wa kudumu  masomo ya sayansi limekuwa likiwahathili hasa pale wanapojikuta kwa mwakammoja wanafundishwa na walimu wanne somo moja ambapo kila mwalimu anakuja na mfumo

Kwa upande wao Exavel Migalambo na Gregoly Bonefas,  walimu wameeleza  kuwa kutokana na tatizo hilo la uhaba wa walimu ni vema serikali ikaweka utaratibu maalum wa kuwapata walimu wa kudumu mashuleni ikiwa ni pamoja na vifaa vya kufundishia

Hata hivyo mmoja wa wahitimu  Juliter Mathias  alisema kuwa pamoja na sekali kuweka utaratibu wa elimu bila malipo kumekuwepo na hali ya baadhi ya wazazi na wanafunzi kutotambua umuhimu huo kutokana na makundi  malika na kueata wazazi walimu na jamaii kwa ujumla kutoa elimu lika ili waweze kujitambua

‘’Pamoja na kuwepo mfumo wa elimu bila malipo jamii imetakiwa kuchangia sekta pale inapo bidi na kuacha kusema kuwa serikali itafanya kila kitu licha ya kuwa watoto ni wa wazazi wenyewe’’ alisema joashi Timoth mzazi, huku mgeni rasmi Padre Andrea Pelamie akiwataka wahitimu kuwa kielelezo katika jamii kama wasomi

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao