Kibondo; Watanzania wametakiwa kujenga tabia ya kuungana na kushirikiana katika shuguli za maendeleo kwenye maeneo yao ili kuweza kufikia malengo yanayokusudiwa bila kuiachia serikali peke yake

Kibondo;  Watanzania wametakiwa kujenga tabia ya kuungana na kushirikiana katika shuguli za maendeleo  kwenye maeneo yao ili kuweza kufikia malengo yanayokusudiwa bila kuiachia serikali peke yake

Akizungumza jana katika kikao cha  Harambee iliyoandaliwa kwa ajili ya kuchingia madawati ya shule za msingi na sekondari Wilayani Kibondo mkoani Kigoma Bw, Philpo Kayanda Afisa Elimu Watu wazima wa Mkoa huo, aliesema kuwa bila jamii kushirikiana maendeleo hayawezi kupatikana

Kayanda aliongeza kuwa watu wengi wamezoea kutoa michango mikubwa kwenye sherehe za harusi na nyinginezo kuliko kusaidia watu wenye matatizo na shughuli za maendeleo hatua ambayo imekuwa ikifanya mambo mengi kuzorota kwa madai kuwa serikali itafanya.

Katika harambee hiyo, wananchi, mashirika ya umma Taasisis za serikali waliweza kutoa michango mbalimbali ili kuziba pengo kubwa la upungufu wa madawati 11,150 huku shule za msingi zinahitaji 17,740 na yaliyopo ni 12 elfu tu pungufu 7720 na sekondari yanaitajika 6000 yaliyopo 3420 tu

Zoezi hilo lilionyesha mafanikio baada ya wadau hao wa elimu kuchanga fedha  tasilim tsh million 13.5 na ahadi  tsh 20 milion,madawati 100 na ahadi ya madawati  6010, huku michango yote ikitarajiwa kukamilisha april 25  

Hata hivyo baadhi ya wakazi wa kibodo,ambapo Bw, Bonefas Buyogela  walipongeza jitiada za serikali kwa kuwashirikisha katika swala hilo na kusema kuwa wanafunzi walioko katika shule zilizoko mkoa wa kigoma hawakutakiwa kukosa madawati kwakuwa mkoa huo una mistu mingi hivyo, upangwe utaratibu maalum wa kutumia rasilimali hizo.

Akitoa shukrani zake mkuu wa wilaya ya Kibondo Bi Ruth Msafiri, alieleza kuwa zoezi hilo pamoja na kufanikiwa kwa kiasi kikubwa, kumekuwepo na changamoto kwa baadhi ya wanasiasa kutoshiriki ipasavyo na kuwataka wote kuacha siasa katika kazi za maendeleo ili kufikia malengo


Nao wanafunzi walipongeza uamuzi wa serikali kuwahamasisha viongozi wa mikoa na wilaya kuliangalia swala la ukosefu wa matawati kwani limekuwa likiwaathili kwa kiasi kukubwa mara wanapokaa chini na wengine kubanana hali ambayo ilifanya kutokuwa huru, na kushusha kiwango cha elimu

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao