Wakati Taifa likiwa katika mchakato wa kuwatambua na kuwaandikisha raia wake kwa ajili ya na kuwapatia vitambulisho, vya Uraia, wananchi hasa wakazi wa Mkoa wa Kigoma, wametakiwa kujitokeza na kuwatambua wahamiaji haramu ili kuepuka kukwamisha zoezi hilo


Emmanuel Maganga Mkuu wa Mkoa wa Kigoma


Luis Bura Mkuu wa wilaya Kibondo

Wakati Taifa likiwa katika mchakato wa kuwatambua na kuwaandikisha raia wake kwa ajili ya  na kuwapatia vitambulisho, vya Uraia, wananchi hasa wakazi wa Mkoa wa Kigoma, wametakiwa kujitokeza na kuwatambua wahamiaji haramu ili kuepuka kukwamisha zoezi hilo

Akiongea na wananchi  wa maeneo mbalimbali ya wilaya ya Kibondo Mkoani Kigoma Mkuu wa Mkoa huo Brigedia General Mstaafu Emmanuel Maganga wakati  wa ziara yake akihamasishaji shuguli za maendeleo   amesema ikilinganishwa na jografia ya mkoa wa Kigoma wamo Raia wa Kigeni ambao wameingia nchini kinyume na Taratibu hivyo wasipowekwa wazi wanaweza kujiingiza katika zoezi hilo

 Amewataka wale wote amabao si Laia wa Tanzania kutojiingiza katoka zoezi hilo  hata kama wao  wanadhani wamezaliwa hapa nchini maana hiyo si sababu ya kuwafanya kuwa watanzania   hata kama wamekaa muda mrefu

''Tunajua kwa ujanja na kutumia fedha mnaweza kutaka kuwa kwenye mpango huo ili nanyinyi muhesabike kama watanzania hilo haliwezekani bila kufuata taratibu za uraia hata kam mzazi wako mmoja ni mtranzia haitakusidia mpaka utakapo ukana uraia wa mzazi mmojawapo na atakegundulika hatua kali za kisheria zitachikuliwa dhidi yake '' alisema Maganga




Mwisho

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao