Kibondo;Kutokana na changamoto nyingi zinazowakabili wanawake, Jamii imetakiwa kulitazama kundi hilo kwa jicho la pekee ili kuondoa kero na kuboresha maisha yao


Kibondo;Kutokana na changamoto  nyingi zinazowakabili wanawake, Jamii imetakiwa kulitazama kundi hilo kwa jicho la pekee ili  kuondoa kero na kuboresha maisha yao

Wanawake ndiyo wenye changamoto nyingi na kundi hili. liko kama vile limesahaulika  lakini ndiyo wenye uthubutu katika kufanya kazi     kukopa na wenye uaminifu wa kulipa fedha kama marejesho ya fedha zinazokuwa zimechukuliwa na makundi yao na kuyataka mashirika. taasisi za serikali na za binafisi kuyatazama makundi ya wanawake kwa Nyanja zote

Kauli hiyo ilitolewa jana  na Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya wilaya Kibondo Mkoani Kigoma Juma Mnwele alipokuwa akifungua washa ya kujenga uelewa kwa maofisa ugani na waratibu elimu ili nao waweze kuwaelekeza walengwa wa mpango wa kusuru kaya kupitia shirika la Tasaf ili kuunda vikundi vya kuweka akiba na kukuza uchumi wao  kupitia shirika la hifadhi ya jamii Tasaf   mafunzo hayo yanafanyika mjini Kibondo

Warsha hiyo imewahusisha maafisa ugani wa kata na  na Waratibu Elimu kutoka katika wilaya za uvinza na kibondo mkoani humo huku mkurugenzi huyo akiwataka kufanya kazi kwa weledi  wakitambua kuwa wameaminiwa kufanya kazi hiyo hivyo na kuwataka kuepuka kuisababishia hasara serikalip

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Tasaf Taifa aliyewakilishwa na ofisa  mafunzo na ushirikishaji Jamii  Catherin  Kisanga, alikili kutambua changamoto hizo  na kueleza  kuwa Tasaf katika mpango wa kunusuru kaya masikini imepata mafanikio na imweza kuzitambua kaya 1369649 na kutekeleza kazi zake katika Vijiji Mitaa na Sheiya 9804 Tanzania bara na Visiwani

Nae  Mratibu wa kitengo cha kuinua uchumi wa kaya masikini  Tasaf makao makuu Ester Kivuyo amesema wanatoa semina kwa washiriki hawa ili wakawaelimishe walengwa namna ya kuunda vikundi vya kuweka akiba na kwa ajili kuweka akiba na kukopeshana kwa ajili ya kujenga uchumi ili kaya hizo ziwe na uchumi endelevu  katika maeneo yao


Baadhi ya washiriki wa maunzo yanaoendeshwa na Shirika la Tasaff yanayofanyika Wilayani  Kibondo


Juma Mnwele  mkurugenzi Halmashauri Kibondo


Ester Kivuyo, Tasaf Makao makuu


Catherin Kisanga  Tasaf Makao makuu

‘’Walioko kwenye mpango hivi sasa ndiyo wanaoruhusiwa kujiunga katika Vikundi hivyo na tuna waelimisha kutumia fedha zile wanazogawiwa  wakati uwwilishaji fedha zinazotolewa kila baada ya miezi tatu na nivizuri wakazitumia vema maana utaratibu huu una mwisho wake  na wafadhili ikitokea wasitisha misahada yao walengwa wabaki na shuguli zao kama kawaida bila kuteteleka’’ alisema Ester

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao