Kakonko;Imeelezwa kuwa kutokana na kukosekana kwa huduma bora kwa wazee ni moja ya sababu zinazochangia kufa kabla ya wakati


Kakonko;Imeelezwa kuwa kutokana na kukosekana kwa huduma bora kwa wazee ni moja ya sababu zinazochangia kufa kabla ya wakati






Licha yasera ya kuwahudumia wazee wenye umri mkubwa bado zipo changamo nyingi zinazowakabili ikiwa ni pamoja na ukosefu  wa chakula mavazi huduma za bora  afya na kusababisha usumbufu mkubwa na manung’uniko yasiyoisha kutoka katika makundi ya ya wazee

Mbonimpa Bisaama ni Mwenyekiti wa chama cha Wazee wilaya ya Kakonko Mkoani Kigoma aliyasema hayo jana wakati wa utoaji misaada kwa wazee 644 wa kata ya Nyamtukuza ambapo alisema wapo wazee wengi wasiyojiweza na wengine wametelekezwa na watoto wao hali inayopelekea kuishi katika Mazingira na magumu na wengine kufa kabla ya wakati wao

Msaada uliotolewa kwa walemavu wenye mahitaji maalumu ni wenye thama ya tsh milion 50.6 kutoka katika shirika lisilokuwa la kiserikali la Help Age ambao ni Magoro, Mashat  Viatu na Blanket huku mkuu wa wilaya hiyo Kanali Hosea Ndagala akisistiza idara ya afya wilayani humo kuhakikisha inawataia Vitambilisho ili waweze kupata huduma za afya bila usumbufu

‘’Kama vifaa vipo kwanini watu wanahidiwa kila mara bila utekelezaji? Tumekuwa kila tunapofika maeneo mengi wazee wanalalamika kutopatiwa vitambulisho na kukosa msaada wa haraka wanapofika maeneo ya kutolea huduma za afaya kwanii sasa naagiza swala hili lifanyike haraka na madirisha kwa ajili ya kuwasaidia wazee yawepo na yafanye kazi’’ alisema Ndagala.

Wilaya ya Kakonko ina wazee wapatao 8000 waliokwishatambulika japo kazi ya utambuzi bado inaendelea ili waweze kupatiwa stahiki zao kama wazee kwa kukumbukwa namna walivyolitumikia Taifa ili na wengine kwa maleze mazuri na kuendelea kutambuliwa michango yao na ushauri katika jamii huku mwakilishi wa shirika laHelp Age lilitoa misada hiyo Janeth Mongi akieleza ili kufikia lengo hilo lazima viongozi wa mitaa kata na Vijiji kushirikiana kulihudmia kundi hilo kwani bado halijapitwa na wakati

Juma Maganga yeye ni mwenyekiti wa Halmashauri ya kakonkoaliwataka wazee hao misaada hiyo kuitumia kwa malengo yaliyokusudiwa wasiuze bali watumia na kutoa taadhali ya wanasiasa ambao wanaweza kuingiza jambo na mambo ya ya Kisiasa
Mwisho       

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao