Wahitimu wa Jeshi la akiba wilayani Kibondo Mkoa wa Kigoma wameiomba serikalikuwapa kipaumbele pale zinapopatikana fulsa za kiulinzi kwa ajili ya kukabiliana na changamoto za ajira na pia kupatiwa mafunzo mbalimbali ya kijeshi ili waweze kujiendeleza na kuwa na ufanisi katika shuguli zao






Wahitimu mafunzo ya awali Jeshi la akiba wakiwa katika Gwaride wakati kufunga mafunzo ya awali

Meja Ahmad Chande Mshauri jeshi la akiba wilaya ya Kibondo

Wahitimu wa Jeshi la akiba wilayani Kibondo Mkoa wa Kigoma wameiomba serikalikuwapa kipaumbele pale zinapopatikana fulsa za kiulinzi kwa ajili ya kukabiliana na changamoto za ajira na pia kupatiwa mafunzo mbalimbali ya kijeshi ili waweze kujiendeleza na kuwa na ufanisi katika shuguli zao

Baada ya kupata mafunzo mbalimbali ya kijeshi na ulinzi na usalama na ujenzi wa Taifa kwa nyanja mbalimbali na kulingana hali halis ya upatikanaji wa ajira na kuomba kupatiwa mafunzo zaidi ili kuongeza uwezo zaidi katika utendaji wao wa kazi

Hayo wameyasema katika katika lisara yao iliyosomwa na Yakin Shedrack wakati wa sherehe ya kufunga mafunzo ya jeshi hilo iliyofanyika katika Kijiji chaa Kumhasa kata ya Mulungu Tarafa ya Kibondo na kueleza kuwa wamejifunza mambo mengi yahusoyo ulinzi

Kwa upande wake Mej Ahamad Chande ambaye ni mshauri wa Jeshi hilo wilaya ya Kibondo kwa niaba ya Mkuu wa wilaya hiyo Luis Bura aliyekuwa amealikwa kama mgerasm amewataka wahitimu hao kutimiza kiapo chao kwa uaminifu ili mafunzo waliyoyapa yaweze kuwa na maana

Aliwataka kuwana utii na nidhamu kwani askali asiyekuwa na nidhamu hafai kulitumikia jeshi la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na anstaili kuondolewa

Nao baadhi ya wahitimu wengine Moshi Hussein na Antifonia Cosmas  waliahitidi kutimiza kiapo na kuenedeka kwa maelekezo ya jeshi hilo na kuwashauri wale ambao hawajapitia mafunzo ya kijeshi kwa kuwaelekeza ili wawe wazalendo

‘’Tutashirikiana na Viongozi wetu wa serikali na kutii amri halali katika vijiji  na kuwa mstari wa mbele katika shughuli za ujenzi wa Taifa kama majanga na maendeleo’’ alisema Moshi
Mwisho



Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao