Burundi waomba Tanzania ushirikiano Mafunzo vyuo vya Uuguzi yaendelee kwa ajili ya kuboresha Taaluma





Proches Kitaronja Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ya Kibondo alipokuwa akiongea na Wageni toka Nchini Burundi Katika Chuo cha Uuguzi Kibondo

Habyalimana Juve Mkuu wa Chuo cha Uuguzi Gisulu




alfreda Ndungulu Mkuu wa Chuo cha Uuguzi kIBONDO

Burundi waomba Tanzania ushirikiano Mafunzo vyuo vya Uuguzi yaendelee kwa ajili ya kuboresha Taaluma

Chuo cha Uuguzi Gisulu  Mkoa wa Chankuzo Nchini Burundi kimeomba ushirikiano wa pamoja katika  kubadilishana uzoefu wa mafunzo ya uuguzi kwa Wanafunzi wan chi hizi mbili

Wakiwa katika ziara ya mafunzo Wilayani Kibondo Mkoani  Kigoma Nchini Tanzania, wanafunzi na walimu kutoka Chuo cha uuguzi Gisulu Mkoani Chankuzo  Burundi, wamesema licha ya Mitaala tofauti katika nchi zao, yapo mambo ambayo yakifanyika kwa kubadilishana uzoefu yaweza kuleta matokeo chanya na kuboresha taaluma hiyo

Habyalimana Juve Mkuu wa Chuo cha Uuguzi Gizulu  amesema wameweza kuona utofauti uliopo katika Vyumba na Vifaa vya kujifunzia kwa njia ya matendo ambapo  kwao hutumia chumba Kimoja wakati wenzao wa Tanzania wanatumia Vyumba kumi na Viwili hatua ambayo wamesema inaondoa changamoto ya ujifunzaji na kuongeza kuwa kwa Burundi Wanafunzi wanatumia muda wa miaka mitatu wakati Tanzania ni miaka minne

Ziara hiyo ya mafunzo Wanafunzi wameleeza tofauti wazoziona katika ujifunzji na namna wagonjwa wanavyopokelewa katika Vituo vya kutolea huduma za afya huku wito kwa Vijana watanzania wakitakiwa kuendelea kujivunia taaluma ya uuguzi kwani ni ya Kimatafa anaeleza Alfreda  Ndungulu Mkuu wa chuo cha uuguzi Kibondo

Awali  ujumbe wa ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kibondo uliotolewa na mwakilishi wa ofisi hiyo, Proches Kitaronja, umewataka Vijana kupenda kujifunza zaidi kwani mambo mengi yamekuwa yakibadilika kuendana na Teknolojia na kusistiza kudumisha mahusiano yalipo kati ya Tanzania na Burundi kwa kuwaendzi wahasisi wan chi hizi mbili kwa kudumisha amani na upendo

 

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao