Uboreshaji wa Elimu unahitaji ushirikiano wa pamoja

 Uboreshaji wa Elimu unahitaji ushirikiano wa pamoja 






Kanali Evance Malasa Mkuu wa Wilaya ya Kakonko alipokuwa akizungunza kwenye hafla ya Makabidhiano ya Madawati na Vitanda vilivyolewa na Benki ya NMB 


Seka Urio Meneja wa NMB Kanda ya Magharibu

Stephan Ndaki Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kakonko







Wakati serikali ikiendelea kuboresha miundombinu ya Elimu Wilayani KakonkoMkoani Kigoma, Mkuu wa Wilaya hiyo Evance Malasa ameitaka jamii kuendelea kushirikiana na walimu ili kuongeza ufaulu kwa Wanafunzi

Maendeleo mazuri ya Mtoto shuleni yanategemeana na ushirikiano wa pamoja kati ya Mwalimu Mzazi au mlezi hivyo wasiachiwe walimu peke yao ameongeza kuwa si vizuri kusika ufaulu Wanafunzi  wa wilaya yao  unendelea kushuka kila kukicha

Malasa aliyasema hayo juzi wakati wa hafla fupi ya kupokea Vitanda na Madawati yaliyotolewa na Benki ya NMB kwajili ya shule ya Msingi Itumbiko  ambapo amesema serikali kupitia wadau wamekuna jitiada za kuboresha elimu hivyo walimu nao hawana budi kutimiza wajibu wao ili kufikia malengo yanayokusudiwa ikiwa ni pamoja naWazazi na  walezi  wa Wanafunzi

Aidha akitoa shukrani zake kwa Benki ya NMB Kanali Malasa alisema kuwa Sekta ya Michezo imesahaliwa na kuagiza Idara husika kulifanyikazi sula hilo kwani ni muhimu katika maisha ya Binadamu  na uboresha afya huku akiiomba Menk ya NMB kuangalia na sekta ya Michezo katika kufadhili vifaa vya Michezo

Benki hiyo imetoa Madawati 150 kwa ajili ya shule za Msingi Nyamtukuza, Kiyogazi na  Itumbiko ambayo imepatiwa Vitanda 50 vyote thamani yake ni Sh  28 Milion kwa ajili ya Wanafunzi wenye Mahitaji  maalum ambapo Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Benson  Woko ameeleza Mikakati waliyonayo kufikia malengo ya serikali

 

Kwa upande wake Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Magharibi Seka Urio alisema kuwa wameamua kutoa msaada huo kwenda na kasi ya serikali kutoa huduma bora ya elimu  na wataendelea kufanya hivyo kwa wilaya ya Kakonko na Mkoa mzima wa Kigoma

Baadhi ya Wanafunzi wa shule ya Itumbiko wametoa shukrani kwa upata Madawati na Vitanda ambavyo vitasaidia kuongeza hali ya ujifunzaji wawapo Darasani pale wanapopunguziwa mbanano na kukaa chini

Mbunge wa Jimbo la Buyungu Aloyse Kamamba yeye licha ya kuipongeza NMB kwa namna inavyojitoa kusaidia sekta ya Elimu hapa nchini amesema wamekuwa wakipokea fedha nyingi kwa ajili ya kuborresha miundombinu ya elimu na sekta zingine ili kupunguza changamoto zinazowakabili Wananchi huku akiishukuru seikali kwa jitiada hizo

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao