Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao

 

 




Maulid Jumaa Mdau wa Elimu na Mkurugenzi Ahava Sekondari alipokuwa akizungumza na wanafunzi na Wazazi wakati wa Mahafali ya pili Kuitimu Kidato cha Nne 

Frolence Samizi Mbunge wa Jimbo la Muhambwe alipokuwa akiwahutubia mamia katika mahafali ya pili kuhitimu Kidato cha nne 2023 Shule ya Sekondari Ahava iliyoko Kibondo Mkoani Kigoma





Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao


Muhingo Mwemezi  Kibondo

Wazazi kutotimiza wajibu sababu zinazopelekea Vitendo vya mmomonyoko wa maadili kuendelea kushamili kwa Watoto na wengine kushindwa kufikia ndoto zao

Licha ya maelekezo toka  kwa Serika na Wadau mbalimbali juu ya  wazazi na walezi ambayo uwataka kutimiza wajibu wao huwaachilia watoto wao katika masuala ya starehe bila maonyo na makaripio kwa watoto na kupelekea kushindwa masomo mwisho wa kwa wasichana kubeba Mimba na wavulana madawa ya kulevya

Baadhi ya wanafunzi wa shule mbalimbali  Wilayani Kibondo Mkoani Kigoma wamesema wengi wao wamekuwa wakikwama kimaendeleo ikiwa ni pamoja na masomo kutokana na wazazi kushindwa kuwapa malezi mazuri licha ya serikali na mashirika kuendelea kuelimisha masuala ya malezi

Jesca Kazuzuzu na Ruth Evance ni baadhi ya Wazazi  nao wanasema kuwa zipo sababu mbalimbali zinazopelekea mmomonyoko wa maadili ikiwa ni wazazi pamoja na Watoto ,,wenyewe

,,Wazazi wengine hawako tayari kuzungunza na Watoto wao kwa kuwaelez  wazi kuanzia masuala ya makuzi na kujiepusha na makundi yasiyofaa hivyo wazazi tunatakiwa kuvunja ukimya tuwasaidie Watoto wawe wasicha au wavulana na sababu nyingine kuvunjika kwa ndoa ambapo wazazi ukosa ushirikiano kuwalea Vijana wao,, alisema Jesca mzazi

Akiwa Mgeni rasmi katika mahafari ya kuhitimu Kidato cha nne shule ya sekondari Ahava Mbunge wa Jimbo la Muhambwe Frolence Samizi amewataka wazazi kuhakikisha wanawaelekeza Watoto wao kuwa na maadili  hadi pale watakapo fikia muda wa kujiunga na kidato cha tano au vyuo

Ndugu wazazi mjielewe kuwa nyinyi ndio mnaotegemewa na Vijana wenu kupata alama nzuri za ufaulu  sikitu kila mmoja ajiulize Mtoto wako anamaliza kidato cha nne je atafika muda  wa kujiunga na kidato cha tano akiwa salama?

Hata hivyo baadhi ya Wasomi wametajwa kuikatisha taamaa jamii kutokana na mienendo isiyofaa kamaa alisema  mmoja wa Wadau wa Elimu  na mkurugenzi shule ya sekondari Ahava Maulidi Juma kwani  usomi wao unavyofikiwa inakuwa tofauti na matendo yao  

Maulidi aliongeza kuwa Serikali imekuwa ikitumia garama kubwa na hasara kutokana na wasomi wengi kutojitambua kwa kukosa uaminifu wa uwajibikaji lakini kutokana na malezi mema na maadili ya kiroho

Alisema katika shule yake wamekuwa wakiwaelekeza watoto kuyashika maadili ya kiroho waweze kukubalika katika mfumo wa ajira wawe na Elimu bora pamoja na maadili mema ya kiroho, hivyo kwani watawajibika ipasavyo tofauti na watu wasiyokuwa na maadili ya Kiroho

Inategemewa Wasomi wafanye mambo mema kulingana na wanavyodhaniwa lakini matokeo yake ni tofauti tunatarajia watuelemishe sisi ila sivyo ilivyo kama ni magonjwa na sababu zake tunategemea elimu kutoka kwa wasomi ila wao ndiyo wanaokwenda kinyume na kupata madila tofauti na watu ambao hawajaenda shule mfano Mtu anafahamu madhara ya uvutaji sigara kitaalam yeye ndiye wa kwanza kuvuta je jamii iatarajie nini kutoka kwa makundi ya wasomi kama si kutukatisha tamaa? Mtaalam anafahamu masuala ya Ngono nzembe ambazo husababisha Magonjwa laikini yeye ndiye mtendaji wa mambo hayo je tutafika? Ikumbukwe kuwa yote hayo ni ukosefu wa elimu ya Kiroho alisema Maulidi Juma

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu