Baadhi ya wanafunzi wa shule mbalimbali za msingi sekondari wilayani kibondo na Kakonko mkoa wa Kigoma wameeleza wasiwasi wao kushindwa kufanya vizuri katika masomo na kukosa ajira baada ya kuhitimu pale serikali ilipotangaza kuwa kuanzia mwakani luga itakayotumika kufundishia itakuwa ni kiswahili badala ya kiingereza tangu shule za awali hadi vyuo vikuu hapa nchini

Wanafunzi wa shule ya sekondari Tutuba wakiwa Darasani
Baadhi ya wanafunzi wa shule mbalimbali za msingi  sekondari wilayani kibondo na Kakonko mkoa wa Kigoma wameeleza wasiwasi wao kushindwa kufanya vizuri katika masomo na kukosa ajira baada ya kuhitimu  pale serikali ilipotangaza kuwa kuanzia mwakani luga itakayotumika kufundishia itakuwa ni kiswahili badala ya kiingereza tangu shule za awali hadi vyuo vikuu hapa nchini

Wakiongea na na Blog hii,
Shani Shaba mwanafunzi tutuba sekondari

Emmanuel Gwegenyeza mtau wa elimu

Sharehe Makunga mkuu shule ya Tutuba sekondari
kwa nyakati tofauti wanafunzi hao ambao ni Shani Shabani,Balosha Josephati  wa shule ya sekondari Tutuba na Georg Gwamagobe wa shule ya Gwegenyeza wamesema kuwa luga iliyozoeleka  na kutumika vizuri katika ngazi zote za elimu ni kiingereza  mara itakapobadirika gafra uende wengi wakashindwa kufanya vizuri kwenye mitihani yao nakuongeza kuwa kama watakuwa wanafahamu kiswahili tu wanaweza kukosa fulsa za ajira hasa katika humuiya ya Afrika masharki na kwingineko

Lugha ni chombo muhimu sana cha mawasiliano kilichoundwa na sauti zanasibu za kusemwa na kutumiwa na jamii ya utamaduni fulani. Jinsi ambavyozipo jamii nyingi za tamaduni mbalimbali duniani, vivyo hivyo ziko lughambalimbali zilizoundwa kukidhi haja ya mawasiliano ya tamaduni mbalimbali.

Maingiliano ya jamii zenye tamaduni na lugha mbalimbali yanayotokana namashirikiano katika shughuli za biashara na nyinginezo za kijamii, huzusha hajaya kuwepo kwa lugha moja itakayoweza kuwaungaanisha watu hao wenye tamaduni na lugha mbalimbali.

Hata hivyo wengine wamekuwa tofauti na wezao kwa kudai kuwa Luga ya kiswahili ni ya asili katika  nchi hii na utaratibu huo unaweza kumfanya mwanafunzi kumuelewa mwalimu ipasavyo

Nao walimu wamekuwa na yao yakueleza kwamba muda ni mfupi sana kuanza kutekeleza hazima kwani inaweza kuchukua muda murefu kubadilisha mitaala hasa katika luga hivyo uenda zoezi hilo likakwama kuzaa matunda kama alivyosema Sarehe Makunga mwalimu toka shule ya sekondari Tutuba

Kuna faida na hasara katika kutumia luga ya kiswahili kufundishia kwani luga hiyo inatumika kwa watanzania wote ni asili ya taifa hili na hata mataifa mengine yanaweza kutafuta watu toka Tanzaniaili wakafundishe kiswahili kwenye nchi zaoalisema Emmanuel Jeremia mkurugenzi wa Shule ya sekondari Gwegenyeza huku mmoja wa wakazi wa kibondo Agnes Katoto akieleza kuwa ni vema utaratibu uendelee kama ilivyo kuwa awali

Na kuongeza kuwa nyakati za hivi karibu elimu katika nchi hii ilishuka kiwango chake kwa wanafunzi kufanya vibaya huku kukiwepo sababu mbalimbali lakini kinachoonekana ni kubadilika kwa mitaala kila wakati hatua inayooneka kuwachanganya wanafunzi.

Joseph Tirutangwa Afisa elimu shule za msingi wilaya ya kibondo yeye amewatoa wasiwasi wananfuzi hao kuwa utakuwepo utaratibu kuhakikisha watu wanafahamu kiingereza na wala tamko hilo la serikali halijasema kuwa luga hiyo haitatumika mashuleni tatizo ni kwamba hata walimu wa sasa hawana mbinu nzuri za kufundisha kiingereza

Aidha Tirutangwa alisema kuwa zipo baadhi ya nchi nyingi dunia zinazotumia Luga zao za asili katika mambo yote ikiwa ni pamoja na kufundishia mashuleni na shuguli zao zinaenda vizuri  

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao