Ukosefu wa kipato cha kutosha na mmomonyoko wa maadili katika familia nyingi hapa nchini ni sababu mojawapo inayowa kupelekea watu wengi kuvunja Taratibu na sheria za nchi katika sekta mbalimbali makazini


Ukosefu wa kipato cha kutosha na mmomonyoko wa maadili katika familia nyingi hapa nchini ni sababu mojawapo inayowa kupelekea watu wengi kuvunja Taratibu na sheria za nchi katika sekta mbalimbali makazini

Wakiongea na Clouds kwa nyakati tofauti baadhi ya wakazi wa mamlaka ya mji mdogo wa Kibondo Mkoani Kigoma wamsema kuwa katika sekta ya usfirishaji wa Abiria na mizigo hususa ni usafiri wa Pikipiki maalufu Bodaboda wamekuwa wakikiuka taratibu na sheria za Barabarani kama kubeba watu zaidi ya mmoja na kubeba mizigo mipana hali ambazo zimekuwa zikipekea kuwepo kwa ajali nyingi za pikipiki

Hata hivyo wameeleza kuwa tatizo kubwa licha ya umasikini ni kuharibika maadili makazini hususa kwa wasimamizi wa taratibu hizo kama polisi wa usalama barabarani kutafanya kwa dhati halinayopekea madhala makubwa katika jamii


Steevin Joka mkuu wa kitengo cha usalama Barabarani kituo cha Polis Kibondo


Jastin Isaka mwendesha pikipiki Kibondo


Nao baadhi waendesha Pikipiki wamedai kuwa pamoja na kuwepo kwa sheria za uendeshaji kuwa hawatakiwi kubeba abiria zaidi ya mmoja tatizoni hali nguvu ya upatikanaji wa fedha kwa jamii wanayoihudumia hali inayopelekea ugumu wa upatikanaji wa fedha katika shuguli zao na kuamua kubeba watu zaidi ya mmoja kama taratibu zinavyoelekeza huku wengine wakisema kuwa hizo ni tamaa na kufanya makusudi kwani hakuna sababu ya kubeba abiria wanne au watatu

Steephan Joka ni mkuu wa kitengo cha usalama Barabarani wilayani Kibondo yeye anaeleza kuwa kama ni elimu uendeshaji wa vyombo vya Moto hasa Pikipiki imekuwa ikitolewa mara kwa mara na kudai kuwa hakuna anayeweza kuwa na kisingizio chochote ila  kinachosumbua ni muingiliano wa siasa ambazo zimekuwa zikisababisha ukiukwaji wa sheria 


Amewata waendesha pikipiki kuwa kama hapo awali katika  kufanya kazi za kwa kuzingatia sheria ili kunusuru maisha ya watu na kuwata abiria kukataa kupakiwa wawili au watatu na kuwataka watembea kwa miguu wawapo barabarani  kupita upande wa kulia ili gari linalokuja mbele liweze kuonekana

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao