Idadi ya wakimbizi raia wa Burundi wanaoendelea kuikimbia nchi yao kutokana na machafuko ya kisiasa yaliyoanza toka mwezi April mwaka jana nakupewa hifadhi katika kambi ya Nduta iliyopo wilayani Kibondo Mkoani Kigoma imeendelea kuongezeka siku hadi siku.

Idadi ya wakimbizi raia wa Burundi wanaoendelea kuikimbia nchi yao kutokana na machafuko ya kisiasa yaliyoanza toka mwezi April mwaka jana nakupewa hifadhi katika kambi ya Nduta iliyopo wilayani Kibondo Mkoani Kigoma imeendelea kuongezeka siku hadi siku.

Hayo ya mebainishwa na mkuu msaidizi wa kambi hiyo Bi Jeska Ntaita alipozungumza na  Clouds fm kuhusiana na idadi ya wakimbizi wanaoendelea kupokelewa kwenye kambi hiyo pamoja na changamoto kwenye kambi hiyo.
Amesema hadi sasa kambi hiyo imepokea zaidi ya wakimbizi 55,500 (hamsini natano elfu na miatano) na kwamba changamoto ya maji iliyokuwa ikiikabili kambi hiyo ikiwa inaendelea kushughulikiwa

Aidha Bi Ntaita amesema kambi hiyo ilisimama kupokea wakimbizi hao kutokana na hapo awali kuwa natatizo kubwa la uhaba wa maji na sasatatizo la hilo la limeshughulikiwa na sasa wana mpango wakuendelea kuwapokea wakimbizi hao hadi kufikia 60,000 ilikupunguza msongamano kwenye kambi zingine zinazoendelea kuwapokea

Baadhi ya wakimbizi wanaoendelea kupokelewa  kwenye kambi ya wakimbizi ya Nduta wilayani Kibondo Mkoani Kiggoma wamesema wanaendelea kuimbia nchi yao kutokana na mauaji yanayoendelea kujitokeza katika nchi yao na sio kwamba wanakimbia njaa kama inavyoelezwa na baadhi ya watu.




Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao