Kibondo;Mkuu wa wilaya ya Kibondo mkoani kigoma Luis Bura amemwagiza mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya hiyo kuwasimamisha kazi watumishi 3 wa idara ya ujenzi kutokana na ubadhilifu wa fedha za ujenzi wa vyumba vya madarasa na nyumba ya walimu katika shule ya sekondari Itaba





Kibondo;Mkuu wa wilaya ya Kibondo mkoani kigoma Luis Bura amemwagiza mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya hiyo kuwasimamisha kazi watumishi 3 wa idara ya ujenzi kutokana na ubadhilifu wa fedha za ujenzi wa vyumba vya madarasa na nyumba ya walimu katika shule ya sekondari Itaba

Watumisha hao wanatuhumiwa kudanganya ili mkandarasi anaejenga nyumba hizo kulipwa milion 109 malipo ya wamu ya pili kwa madai kuwa ujenzi umekemilika kwa asilimi 85% ambapo milion 46 zimelipwa bila kufanyiwa kazi yoyote huku ujenzi ukiwa chini ya viwango na ukiwa uko chini ya asilimia 50% kama alivyoeleza mkurugenzi wa halmashauri hiyo Juma Mlehe kwa waandishi wa habari na wananchi

Mkuu huyo wa wilaya katika maelezo yake alisesema matatizo ya ubadhilifu wa fedha za serikali katika wilaya hiyo yamekuwa ni mambo ya kawaida huku akilalamikia makundi ya wanasiasa kuingilia shughuli za kitaalam kwa kuwalazimisha watumishi wa halmashauri kufanya  mambo wanayoyataka wao  na kuwataka kufuata sheria na taratibu

Aidha Bura, alisema baada kupata malalamiko ya vitendo vinavyofanywa na mkandara, waandisi walmashauri na baadhi ya wanasiasa, kamati ya ulinzi na usalama ilifika katika eneo la ujenzi na kukuta kile kilichodaiwa kuwa ujenzi umekamilika sivyo ilivyo kukuta vyoo ni mashimo madirisha hayapo sakafu haijawekwa na kuamua mwaandisi  Salehe Mbogoye, Felix Ngomano na Haruni Mbapaye

‘’Madiwani hawa juzi waliomba posho ya kufanya ukaguzi wa ujenzi huu wakapewa posho ya siku tano na hata kwenye ujenzi hawakufika hadi leo jamani mambo hayo ni aibu, na kuongeza kuwa wengine wanaoangukiwa na mkasa huo ni na kutakiwa kuandika barua za maelezo ni Afisa elimu sekondari Wilaya Honolata Kabundugulu,Fedy Eliasafu afisa maliasili na Afisa kilimo wilaya Said Shemahonge nazitaka barua hizo jumanne kwenye kikao alisema Bura’’     

Hata hivyo viongozi wa vijiji mmoja wao Bosco Ngomagi wameiomba serikali kuhakikisha wanashirikishwa mara miradi inapoingizwa katika vijiji vyao ili ufuatiliaji na ushauri uweze kufanyika kwa ukaribu huku vibarua na mafundi waliopewa kazi na kampuni iliyochukua kandarasi  iliyofahamika kwa jina la Mangalazi engnearing ya mjini kigoma  wakiomba msahada wa ufuatiliaji wa amalipo yao kwa kuwa fedha nyingi zimeshachukuliwa alieleza Paschal Leonard

Ujenzi huo  unagarimu shilingi million 264 kwa  ajili ya ujenzi wa nyumba ya walimu yenye kuchukua familia sita Vyumba vitatu vya madarsa, vyoo vitatu vya kisasa kwa ajili ya wanafunzi na walimu matundu mawili ambapo vyote hivyo bado havija kamilika licha ya kudaiwa kuwatayari

Katika uchunguzi mdogo uliofanywa na Gazeti la Mwananchi umebaini wapo baadhi ya madiwani ambao wamekuwa wakiwashawishi baadhi ya watumishi wa halmashauri kuwapa  fedha na wanapokataliwa uanza kuwaandama kwa kuwaadhimia kwa madai watua hao hawafai na kutaka wahame au wasimamishwe kazi  hali ambayo uenda ndiyo inayopelekea wengi wao kutofuata taratibu 

Mwisho

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao