Wakati jamii nyingi zikihangaika kuhakikisha watoto wao wanapata elimu kwa namna yoyote ile, hali imekuwa tofauti kwa baadhi ya wazazi wengine ambao wamewakikataa watoto wao kuendelea na elimu ya juu kwa madai wao ni masikini



Wakati jamii nyingi zikihangaika kuhakikisha watoto wao wanapata elimu kwa namna yoyote ile, hali imekuwa tofauti kwa baadhi ya wazazi wengine ambao wamewakikataa watoto wao kuendelea na elimu ya juu kwa madai wao ni masikini

Amos Mabula ambae ni mwalimu mkuu wa shule ya Nyakasanda , iliyoko Tarafa ya Mabamba wilayani Kibondo Mkoa wa Kigoma,  alipokuwa akiongea na clouds Tv, amesema kutokana na mwamko mdogo wa elimu, miongoni mwa baadhi ya wazazi, wamekuwa wakiwazuia watoto kufanya vizuri kwenye mihani yao kuhitimu elimu ya msingi kwa kisingizio kuwa wakifaulu wao hawana uwezo wa kuwasomesha

Amesema kutokana na hali hiyo baadhi ya wanafunzi wamekuwa wakichora picha za wanyama kwenye karatasi za kujibia mitihani japo majina yao uandikwa kwa usahii 
Afisa elimu shule za msingi wilayani humo Joseph Tirutangwa, alipotembelea shule hiyo na kuongea  baadhi jamii amewataka kuachana na mawazo potofu kwani hali hiyo ni kuharibu maisha ya watoto wao

Hata hivyo mmoja wa wazazi Jacob Madaha,  katika hatua ya kuelimishana, wakati mahafali ya kuhitimu kidato cha nne katika shule ya sekondari Bon consilii iliyokoko katika tarafa hiyo amewambia wazazi hao kuwa wanapaswa kwenda na mabadiliko ya ulimwengu kwani mzigo wanao ukataa unaweza kuwaelemea zaidi hapo baadae pale wasipowasomesha watoto wao

Nao baadhi ya wanafunzi wamekuwa na maoni mitazamo mbalimbali wakiiomba serikali kulingana na mazingira zinakoishi baadhi ya jamii ni bora zikawa zinatembelwa kaupewa elimu kwa ajili ya kunusulu vizazi vijavyo huku wakiwataka wanafunzi kujitambua wao wenyewe

Mwisho

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao