Kibondo;Wanaufaika wa mpango wa kunusulu kaya masikini kupitia Tasaf wametakiwa kujitathimini tangu wameanza kupokea fedha mpango huo ni mambo gani waliyoyafanya kulingana na malengo ya serikali ya kuhakikisha wanapiga hatua moja hadi nyinginewaka

Wanufaika wa mpango wa kunusulu kaya masikini
Luis Bura mkuu wa wilaya kibondo



Beatrice Joseph mwezeshaji Tasaf Kibondo

John Makunja kaimu mratibu Tasaf Kibondo

Kibondo;Wanaufaika wa mpango wa kusulu kaya masikini kupitia Tasaf wametakiwa kujitathimini tangu wameanza kupokea fedha mpango huo ni mambo  gani waliyoyafanya kulingana na malengo ya serikali ya kuhakikisha wanapiga hatua moja hadi nyingine

Hayo ameyasema Mkuu wa wilaya Kibondo Mkoani Kigoma Luis Bura wakati zoezi la ugawaji fedha kwa walengwa wa mpango huo ambapo alisema hivi sasa awamu ya kwanza inaelekea ukingoni ili watoke na wengine waingie na kunuaika

Alisema kwa wale ambao hawakuanikiwa kufikia malengo yao bado hawajachelewa kwa kipindi kilichobaki  hivyo wanatakiwa kuwa makini kwakuzitumia vema pesa hizo

John Makunja yeye ni kaimu mratibu wa Tasafu Kibondo amesema tatizo la watu waliokwama kufikia lengo si kubwa sana lakini wamekuwa wakiendelea kuwaelekeza namna ya kuzitumia fedha hizo na kuongeza kuwa katika kipindi cha mwezi Julai agast fedha zilizotolewa ni tsh  301 milion

Nao baadhi ya wanufaika wa mpango huo ambao ni Sanilwa Binyago,Editha Masabo na Ndabandi Abeli walisema kuwa  kusaidiwa na mpanguon kujenga za kuishi  waliokuwa na nyumba za majani waliweza kuzibadilisha ikiwa ni pamoja na kukua miugo kama kuku na mbuzi ikilinganishwa na hali zao za awali ambapo hata kupata chakula ilikuwa shida

Kwa upande wake mwezeshaji  wa wanufaika wa  mfuko  wilaya ya kibondo Beatrice Joseph alisema changamoto zilizopo ni chache kwa  walengwa kutotimiza masharti hasa kwa kuwapeleka watoto Clinic na Mashulen

Mwisho

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao