Mkutano wavunjika wananchi wakidai hadi Diwani wao aliyepotea katika mazingira ya kutatanisha, wapewe maelezo yake alipo

Kibondo;Wananchi wa kijiji cha kagezi kata ya kagezi wilayani kibondo mkoani kigoma wamegomea mkutano wa serikali ya kijiji kuendelea baada ya kuibuka hoja wakitaka kujua diwani wa kata hiyo ambae pia ni mwenyekiti wa halimashauri ya wilaya hiyo .Simoni Kanguye anayedaiwa kupotea katika mazingira ya kutatanisha.

Diwani wa Kata hiyo Simon Kanguye ambaye pia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya Kibondo anadaiwa kupotea katika mazingira ya kutatanisha tangu julai 20 mwaka huu bado hapatikana licha ya juhudi kubwa za vyombo vya ulinzi kumtafuta

Wakizungumza katika mkutano huo  uliofanyika Kijijini hapo jana baadhi ya wananchi ambao ni Stephan Ntabindi na Juma Bilampanye walisema hawaoni haja ya kuendelea na ajenda nyingine na kujadili maendeleo ya kijiji chao kwaku wa hawana kiongozi ambae atawafikishia kero,na hoja zao katika ngazi husika hadi watakapopewa ufafanuzi.

‘’Hatuwezikujadili maendeleo bila msimamizi maana hata kero zetu tukizitoa hapa hakuna mtu wa kutuwasilishia na hakuna wa kusimamia miradi hiyo ya maenedeleo hivyo hatuko tayari kuendelea na mkutano huu ahdi tupewe maelezo Diwani wetu kama aliungwa au alifariki dunia’’ alisema Juma
Licha ya mtendaji wa kijiji hicho Shaban Mohamed kuwataka wananchi hao  kutulia ili wajadili maendeleo ya kijiji chao. walikataa mkutano huo kuendelea ambapo walimtaka mtendaji wa kata Apolinaly Stephen kutoa maelezo

Hata hivyo  mtendaji huyo wa kata alisema yeye hana maelezo yoyote  kwa sababu nafasi yake ni ndogo juu ya hilo huku mwenyekiti wa kijiji Zabron Ntimba akisema kuwa swala hilo mwenye uwezo wa kulisemea ni mkuu a wilaya ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya kuwataka kuendelea hatua iliyosababisha mzozo  mkali

Pamoja na kupewa maelezo kuwa wanatakiwa wajadili namna ya kushiriki ujenzi wa zahanati ya kijiji kwakuwa wamepata mfadhili wasije wakapokonywa msahada huo walikataa katakata hali iliyopelekea mwenyekiti kufunga mkutano baada ya mzozo kuwa mkubwa


Mmoja wa wananchi walokuwa wakilalamikia upotevu wa Diwani wa Kata ya Kagezi

Shaban Mohamed mtendaji wa Kijiji Kagezi

Zabron Ntimba mwenyekiti Kijiji Kagezi

‘’Hilo jambo ni kubwa sisi ngazi ya kijiji hatuwezi kulitolea maelezo naomba tuliache tuendelee na agenda zetu maana hilo si moja ya ajenda zetu mmeliingiza bila utaratibu na kwakuwa mmekataa tusiendelee, basi msimlaumu mtu pale kazi zitakapokuwa zimekwama alisistiza Ntimba mwenyekiti wa Kijiji’’

Mkuu wa polisi mkoa wa kigoma redinad Mtui hivi karibu alipokuwa akiongea  waandishi wa habari juu ya kupotea kwa mwenyekiti huyo. Alisema kuwa haiahamiki alipotelea wapi ila baada ya oisi yake kupata taarifa za kupotea kwake wajitahidi sana kumtafuta bado hajapatika japo bado jitiada zinaendelea kuhakikisha anapatikana 



Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao