Waumini wa Dini ya Kikristo na jamii kwa ujumla wametakiwa kufuata maadili ya mwenyezi Mungu kwa kuwa na upendo na kuwajali wengine ikiwa ni pamoja na familia na wote wasiyojiweza na kuondoa matabaka na kuhamsishana kufanya kazi








Waumini wa Dini ya Kikristo na jamii kwa ujumla wametakiwa kufuata maadili ya mwenyezi Mungu  kwa kuwa na upendo na kuwajali wengine ikiwa ni pamoja na familia na wote wasiyojiweza na kuondoa matabaka na kuhamsishana kufanya kazi

Wito huo umetolewa na Padre Simon Libeio ambaye ni Paroko wa Parokia ya Kalinzi Kigoma wakati wa Ibaada maalum iliyofanyika Parokia ya Mabamba Kimbondo kwa ajili ya  Watawa wa Kike waliopata Daraja hilo ambapo amesema jamii nyingi hapa nchi zimepungukiwa upendo wa kumpenda Mungu na wanadamu ahli inayopelekea watu wengi kutojali familia na kuzama katika mambo ya utandawazi

Simon ameongeza kuwa Wazazi wengi wameacha wajibu wao wa malezi  kwa watoto hali inayopelekea kuwa na kizazi kisichokuwa na maadili hapo baadae huku baadhi ya waumini walioshiriki Ibada hiyo wakieleza kuwa kinachopelekea kuwepo hali hiyo ni ukosefu wa Imani na kutoka kufanya kazi ya kuongeza kipato cha familia na kupelekea umoja kutoweka

Hata  hivyo swala la mmomonyoko wa maadili umekuwa ukisukiwa kwa vijana na baadhi ya wazazi ambapo baadhi ya vijana wilayani Kibondo wamesema tatizo hilo liko vijana licha ya baadhi ya wazazi kutoa maelekezo ya makuzi na huku wengine wakiwalaumu baadhi ya wazazi kuwabagua watoto wa kike

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao