Kibondo;Migogoro mingi na mikubwa yakugombania ardhi hapa nchini, imetajwa kusababishwa na uelewa ndogo kwa jamii juu ya matumizi na umiliki wa ardhi kwa kuzingatia utawala wa sheria


Washiriki wa semina juu sheria ya umiliki wa ardhi


Nichoraus Ntiayagila mwanasheria Halmashauri ya Kibondo aliyekuwa mkufunzi katika semina hiyo

Padre Andrea Kelemiye Parokia ya Mabamba

Kibondo;Migogoro mingi na mikubwa yakugombania ardhi hapa nchini, imetajwa kusababishwa na uelewa ndogo kwa jamii juu ya matumizi na umiliki wa ardhi kwa kuzingatia utawala wa sheria

Kutokana na hali hiyo, ili kuzuia na kupunguza malumbano katika jamii, Kanisa Katholic Jimbo la Kigoma jana   limeamu kutoa mafunzo kwa muda siku mbili kwa wenyeviti , Watendaji wa kata na vijiji ili waweze kufahamu sheria ya umiliki wa ardhi kama anavyoleza Padre Andrea Kalemiye kutoka Parokia ya Mabamba wilayani Kibondo

‘’Kumekuwepo  na migogoro ambayo haina sababu  na kupelekea watu kusababishiana madhala ya kuuwana na kuitilafiana kati ya Mtu na mwenzake Mtu na Taasisi hivyo tumeona tuweke mafunzo haya ili watu hasa viongozi wa Vijiji wafahamu jinsi ya kutatua migogoro ya ardhi kisheria ailisema Kelamiye ‘’Paroko Parokia ya Mambamba

Mkufunzi  wa mafunzo hayo Nichoraus Ntiyagila ambaye ni mwanasheria Halmashauri ya Kibondo, amesema kutoka na viongozi wengi katika ambako ndiko jamii kubwa iliko hasa kwenye mabaraza ya ardhi kumekuwa kukifanyika mambo yasiyo hama kwa makusudi au kwa kutokujua na kusisitiza kuwa kila mtuapaswa kujua anatakiwa kufuata sheria

Aidha Ntiyagila alisema kuwa maeneo mengi Vijijini  na maeneo yenye madini watu wamekuwa wakishindwa kuafahamu ardhi ni nini na ni vitu gani vinavyo  sababisha ardhi na ni vitu gani ambavyo mtu anaruhusiwa kisheria kuvimiliki yeye binafi si kama madini, Mafuta na Gesi ambapo haijuishwi katika ardhi na kuanza kugombania wengine kwa kufahamu au kwa makusudi

Nao baadhi ya washiriki walisema kuwa wameongezewa maarifa hasa kwa maswala ya utatuzi wa migogoro ya ardhi kwa kuzingatia sheria kwa kuwa tangu wamechaguliwa hawakuweza kupata maelekezo kama hayo na kuahidi kutumia elimu hiyo mara watakapo kuwa katika vituo vyao vya kazi

Wilaya ya Kibondo ilianzishwa mwaka 1954 na ilipofika mwaka 2012 baadhi ya maeneo yake yaligawanywa na kuunda wilaya mpya ya Kakonko, ambapo kwa sensa ya mwaka 2012 wilaya ya kibondo ilikuwa na Idadi ya Watu 261,331 huku tangu kuanzishwa kwake hadi mwaka huu ilikuwa ina hati 60 tu za watu wanaomiliki  ardhi

Nae Mbunge wa Jimbo la Mhambwe wilayani humo Atashasta Nditiye yeye amongeza kuwa ili  kuondoa migogoro ya ardhi ndani ya jamii serikali ina mpango wa kupima ardhi na kutoa hati kwa wamiliki kwa nchi nzima nzima na kibondo ikiwemo hatua itakayoondoa malumbano na kuwafanaya wananchi kunufaika na ardhi yao
Mwisho

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao