DKT. BITEKO: RAIS SAMIA AENDELEA KUENZI MAONO YA HAYATI MAGUFULI KWA VITENDO

 

































DKT. BITEKO: RAIS SAMIA AENDELEA KUENZI MAONO YA HAYATI MAGUFULI KWA VITENDO

Maono ya aliyekuwaRais wa Awamu ya Tano, HayatiDkt. John PombeMagufuli katika utekelezaji wa miradimikubwa ya Kitaifa kama Ujenzi wa Bwawa la Nyerere, Ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR), Ujenzi wa barabara namadarajamakubwa kama vile Daraja la Kigongo - BusisiyametekelezwanayanaendeleakutekelezwanaSerikali ya Awamu ya SitainayoongozwanaRais, Dkt. SamiaSuluhu Hassan.

Hayo yameelezwaNaibu Waziri Mkuuna Waziri wa Nishati, Dkt. DotoBiteko katika Misa Takatifu ya kumuombeaRais wa Awamu ya Tano, HayatiDkt. John PombeMagufuli, iliyofanyika katika KanisaKatolikiParokia ya Mtakatifu Yohana Maria MuzeyiWilayaniChatoMkoaniGeita.

“NiwahakikishieWatanzaniza kuwa miradiyoteambayoHayatiDkt. MagufuliakiwaRais wa Nchi yetu, Serikali ya Dkt. SamiaSuluhu Hassan inaiendelezayote kwa kasikubwailitumuenzi kwa vitendo”, amesemaDkt. Biteko.

Dkt. Bitekoameeleza kuwa WatanzaniawatamkumbukaHayatiDkt. John PombeMagufuli kwa uwezo wake wa kiuongozi, karamayake ya kutatuachangamoto za wananchi pamoja nakuwasikiliza, kuondoakeromahalipenyekero, kuhimizauwajibikajiSerikalini kwa kuondoauzembe, ubadhirifunarushwa.

Katika Misa hiyo, Naibu Waziri MkuuDkt. DotoBitekoameongozaharambee ya kuchangia ujenzi wa kanisajipya la Mtakatifu Yohana Maria MuzeyinanakuwezakukusanyatakribaniMilioni 169 pamoja na vifaa vya ujenzi.

Kwa upande wake, Waziri wa Ujenzi, Innocent BashungwaamemshukuruMhe. RaisDkt. SamiaSuluhu Hassan kwa kumpa nafasi ya Uwaziri katika Wizara ya Ujenzi ambayoHayatiDkt. John PombeMagufulialihudumiamiaka 20.

Naye, Mkuu wa Mkoa wa Geita, Martine ShingellaamemshukuruRaisSamia kwa kutimizandoto za HayatiMagufuli za kujenga barabara kuunganishaMkoa wa GeitanaShinyanga kwa kiwango cha lamiambapotayariSerikaliimesainimtakataba wa ujenzikilometa 73 kwa kiwango cha lamikuanziaKahamahadiKakola.

Kwa niaba ya Famia ya HayatiMagufuli, JescaMagufuli, amemshukuruMhe. RaisDkt. SamiaSuluhu Hassan kwa kuwa karibunafamiliakuwafariji, kuwajalinakuwapatiamatunzoyotekadriawezavyo.

Jescaameongeza kuwa kama familiawataendeleakumuenzinakumkumbukaHayatiDkt. Magufuli kwa namnaalivyowapendanakuwawekea misingi mizuri ya kuchapakazinakumtanguliza Mungu mbele kwenye kilajambo.

Misa ya Kumbukizi ya MiakaMitatutangualipofarikiHayatiDkt. John PombeMagufuliimeongozwanaMakamuAskofu, PadriOvanMwengenakuhudhuriwanaviongozi wa Serikali, Chama cha Mapinduzi (CCM), ndugu, jamaanamarafiki.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao