PAC YAKAGUA MRADI WA UBORESHAJI KIWANJA CHA NDEGE TABORA

 




PAC YAKAGUA MRADI WA UBORESHAJI KIWANJA CHA NDEGE

TABORA


Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) imetembelea

na kukagua mradi wa ukarabati na uboreshaji wa Kiwanja cha ndege cha

Tabora unaotekelezwa na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS).

Kamati hiyo ikiongozwa na Makamu Mwenyekiti wa Kamati, Mheshimiwa

Japhet Hasunga (Mb), ikiwa mkoani Tabora Machi 17, 2024 imeshauri kwa

Wakala huo masuala mbalimbali ikiwemo kumsimamia Mkandarasi

kuongeza kasi ya utekelezaji wa mradi huo ili wananchi wa Tabora na

mikoa jirani waweze kunfaika na mradi huo.

"Msimamieni Mkandarasi aongeze kasi ya utekezaji wa mradi ili ukamilike

kwa wakati, nao wananchi wa Tabora na mikoa jirani waweze kufurahia

huduma ya usafiri wa anga", amesema Hasunga.

Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Ludovick

Nduhiye amesema Wizara imepokea ushauri na maelekezo ya Kamati na

kuahidi kuyafanyia kazi kwa manufaa ya jamii na Taifa kwa ujumla.

Awali akiwasilisha taarifa ya mradi huo, Mtendaji Mkuu wa

TANROADS, Mhandisi Mohamed Besta amesema Mradi huo umefikia

asilimia 38 na unahusisha Ujenzi wa Jengo la abiria litakalohudumia abiria

120 kwa wakati mmoja, Mnara wa kuongoza ndege, barabara ya kuingia

na kutoka kiwanjani pamoja na ujenzi wa uzio wa usalama wenye urefu wa

kilometa 6.25

Mradi wa Uboreshaji na Ukarabati wa Kiwanja cha Ndege cha Tabora

utagharimu Tsh. Bil. 24 na unatarajiwa kukamilika tarehe 11 Oktoba 2024.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao