WAZIRI BASHUNGWA AAGIZA WAHANDISI WASHAURI WANAOSHINDWA KUSIMAMIA MAKANDARASI KUTOPEWA KAZI

 





WAZIRI BASHUNGWA AAGIZA WAHANDISI WASHAURI WANAOSHINDWA KUSIMAMIA MAKANDARASI KUTOPEWA KAZI

Waziri wa Ujenzi, Innocent BashungwaameiagizaWakala wa Barabara (TANROADS) kutowapatiakazi za usimamizi wa miradiWahandisiWashauriwanaoshindwakuwasimamiaWakandarasikutekelezamiradi ya ujenzi wa barabara kwa viwangonamujibu wa mikatabanakupelekeaMkandarasikurudishwaeneo la mradi kurudiakazi.

Bashungwaameagiza hayo Machi 22, 2024 Wilayani Mafia wakati akikagua barabara ya Kilindoni -  Utende (km 14.6) kwa kiwango cha lami, iliyojengwanaMkandarasi CHICO nachini ya usimamizi wa Mhandisi Mshauri Kampuni ya UWP Tanzania ambapo barabara hiyohaikutekelezwa kwa viwangonakusababishaMkandarasikurudia sehemu ya kazi.

“Kama mlivyofanya katika mradi huu kwa kumrudishaMkandarasi Site, WahandisiWashauri kama hawawanaoshindwakumsisimamiaMkandarasiwanapaswawawe ‘blacklisted’ kwa sababutunawalipapesa ya kumsimamiaMkandarasikwaniaba ya Serikali”, amesemaBashungwa.

BashungwaamemuagizaMtendajiMkuu wa TANROADS kutompatiakaziyoyote ya kusimamia miradiMhandisi Mshauri wa kampuni ya UWP Tanzania nawahandisiwashauriwengine wa ainahiyoambaowameshindwakutekelezawajibuwao kwa kuwasimamiaMakandarasikutekelezamiradikikamilifunakuisababishiahasaraSerikali.

“Mhandisi Mshauri UWP hafainanikionammempakazi sehemu yototemiminanyinyina hii iwefunzo kwa WahandisiWashauriwenginetunaowapakazi ya kuwasimamiaMakandarasi”, amesemaBashungwa.

Aidha, Bashungwaamesema kuwa Wizara ya Ujenzi itaendeleakuwasimamiaWakandarasinaWahandisiWashauriwalipatiwakazi za kutekelezamiradiilifedhazinazotolewanaMheshimiwaRais, Dkt. SamiaSuluhu Hassan ziwezekutekelezanakukamilishamiradikikamilifu kama ilivyokusudiwa.

Naye, KaimuMkurugenzi wa Miradikutoka TANROADS Eng. MalimaKusesaameeleza kuwa ujenzi wa barabara ya Kilindoni - Utende (km 14.6) kwa kiwango cha lamiulikamilikamwaka 2015 nabaada ya muda wa matazamio 2016 yalibainikamapungufu katika kipande cha kilometanne.

Eng. Kusesaameeleza kuwa baada ya kubainikamapungufu hayo,TANROADS walimtakaMkandarasi CHICO naMhandisi Mshauri UWP Tanzania kurudiakazi sehemu hiyo kwa gharama zao.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao