Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Aprili, 2026

DC KIGOMA AWATAKA WANANCHI KULINDA MAZINGIRA KWA KUTUMIA NISHATI SAFI

Picha
  FROLENCE  MASUNGA MWAKILISHI ENVOTEC Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Dkt. Rashid Mohamed Chuachua, ametoa wito kwa wananchi wilayani humo kumuunga mkono Rais Samia Suluhu Hassan, kwenye ajenda ya matumizi ya nishati safi ya kupikia ili kulinda na kuhifadhi mazingira. Rashid Chuchua Dc Kigoma Dkt. Chuachua ametoa wito huo wakati wa akizindua ugawaji wa majiko sanifu ya kupikia ya gharama nafuu yenye ruzuku ya serikali, kwa wananchi katika kata ya Simbo wilayani Kigoma, ambapo amesema kuwa matumizi ya majiko sanifu ni hatua muhimu ya kubana matumizi na zaidi kulinda na kuhifadhi mazingira, kwa kuwa majiko hayo yanatumia nishati kidogo. Kampuni ya ENVOTEC iliyopewa dhamana ya kuuza majiko hayo kwa bei ya ruzuku kupitia Wakala wa Nishati Vijijini REA, kwa ujumla imegawa majiko 1,404 kwa wilaya ya Kigoma, ambapo mwakilishi wa kampuni hiyo Florence Masunga, amesema wananchi watachangia asilimia 15% tu ya bei huku serikali ikilipia asilimia 85%. . Baadhi ya wananchi waliopata majiko...

KATIKA KUKABILIANA NA MAJANGA YA MOTO SERIKALI IMETOA GARI LENYE MTAMBO WA KUZIMIA MOTO KATIKA WILAYA YA KIBONDO

Picha
  Wilaya ya Kibondo mkoani Kigoma imepokea gari (mtambo) utakaosaidia katika kukabiliana na majanga ya moto yanapotoke Uzinduzi wa mtambo umefanyika ofisi ya mkuu wa wilaya ya Kibondo ambapo mkuu wa wilaya hiyo Kanali Aggrey Magwaza amesema mtambo huo utasaidia kwa kiasi kikubwa hasa pale zitakapotokea changamoto za ajali za moto Aidha ameagiza uongozi wa halmashauri chini ya mwenyekiti wa halmashauri Bw. Alex Baragomwa kuhakikisha wanatoa ushirikiano kwa zimamoto katika upatikanaji wa maji, mafuta na matengenezo ya mtambo huo ili uendelee kutoa huduma katika hali ya ubora Awali kaimu Kamada wa jeshi la zimamoto na uokoaji mkoa wa Kigoma Mrakibu masaidizi Michale Maganga amesema imani yake ni kwamba, kuwepo kw amtambo huo kutawafanya wananchi wa wilaya ya Kibondo wawe salama zaidi dhidi ya majanga ya moto Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Kibondo Bw. Alex Baragomwa pamoja na mwenyekiti wa chama cha mapinduzi wa wilaya hiyo Bw. Hamisi Tahiro wameomba elimu izidi kutolew...

UKARABATI WA MELI YA MV LIEMBA MKOANI KIGOMA WAFIKIA 64%

Picha
  Dkt Rashid Chuachua Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Serikali ya Tanzania yaendelea kukarabati Meli ya Mv Liemba ambayo imekuwa ikifanya shughuli zake katika Ziwa Tanganyika na zoezi hili linafanyika Mkoani Kigoma [engo ikiwani kuboresha huduma za usafiri wa Majini kwa Wananchi wa Mwambao wa Ziwa Tanganyika na Nchi jirani za Burundi Congo DRC na Tanzania Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Balozi Simon Sirro, amemshukuru Rais wa JamhurI ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kutoa fedha zaidi ya Shilingi Bilioni 32 kwa ajili ya ukarabati mkubwa wa Meli ya Kihistoria ya Mv.Liemba. Shukrani hizo za Mkuu wa Mkoa Balozi Simon Sirro kwa Rais, zimetolewa kwa niaba yake na Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Dkt. Rashid Chuachua, wakati alipomwakilisha kwenye mapokezi ya Injini mbili zilizofika kwa ajili ya kukamilisha ukarabati mkubwa wa Meli ya Mv.Liemba katika Bandari ya Kigoma. Amesema hatua hiyo inaashiria historia mpya kwa wana Kigoma kwenye sekta ya usafiri na usafirishaji katika Ziwa Tang...

KIBONDO YAENDELEZA KAMPENI KUUNGANISHA WATOTO WANAOISHI MITAANI NA FAAMILIA ZAO NA WENGINE KURUDISHWA MASHULENI

Picha
  Aneth Kolman Mkuu wa Dawati la Jinsia Jeshi la Polis Kibondo Sophia Gwamagobe Afisa Ustawi wa Jamii Wilaya ya Kibondo Mkoani Kigoma Lukas Lazaro mwakilishi wa Mkurugenzi Halmashauri ya Kibondo Skola Kachiila Mkazi wa Kibondo Elias Jackson Mkazi wa Kibondo Kuendelea kuwepo Watoto wanaofanya kazi na kuishi mitaani, hali hiyo imetajwa kuchochewa na baadhi ya Wazazi kutumia ukali zaidi katika kuwakanya, migogoro ya familia, umasikini na utukutu wa watoto wenyewe mambo hayo hupelekea kutoroka katika familia na kuishi mitaani Wengi wa Watoto hao wanapoingia Mitaani huanza kufanyabiashara za kuokota na kuuza chupa za plastic na Vyuma chakavu na wengine kazi za majumbani na wanaokosa shughuli hujuhusisha na udokozi hatua ambayo ni hatari kwa maisha yao maana wengi wao ni wanakuwa na umri mdogo Hayo yamebainishwa katika maadhimisho ya Mtoto anaeishi na kufanya kazi mitaani ambapo Afisa ustawi wa jamii wilaya ya Kibondo Kigoma, Sophia Gwamagobe ameeleza kutokana hali hiyo watoto huroka...