UKARABATI WA MELI YA MV LIEMBA MKOANI KIGOMA WAFIKIA 64%
![]() |
| Dkt Rashid Chuachua Mkuu wa Wilaya ya Kigoma |
Serikali ya Tanzania yaendelea kukarabati Meli ya Mv
Liemba ambayo imekuwa ikifanya shughuli zake katika Ziwa Tanganyika na zoezi
hili linafanyika Mkoani Kigoma [engo ikiwani kuboresha huduma za usafiri wa
Majini kwa Wananchi wa Mwambao wa Ziwa Tanganyika na Nchi jirani za Burundi
Congo DRC na Tanzania
Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Balozi Simon Sirro, amemshukuru
Rais wa JamhurI ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kutoa
fedha zaidi ya Shilingi Bilioni 32 kwa ajili ya ukarabati mkubwa wa Meli ya
Kihistoria ya Mv.Liemba.
Shukrani hizo za Mkuu wa Mkoa Balozi Simon Sirro kwa
Rais, zimetolewa kwa niaba yake na Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Dkt. Rashid
Chuachua, wakati alipomwakilisha kwenye mapokezi ya Injini mbili zilizofika kwa
ajili ya kukamilisha ukarabati mkubwa wa Meli ya Mv.Liemba katika Bandari ya
Kigoma.
Amesema hatua hiyo inaashiria historia mpya kwa wana
Kigoma kwenye sekta ya usafiri na usafirishaji katika Ziwa Tanganyika, baada ya
miaka kadhaa ya kusimama kwa Meli ya Mv.Liemba bila kutoa huduma.
Meneja Mradi wa Ukarabati wa Meli ya Mv. Lemba
Mhandisi Elias John Kivala, ukarabati wa meli hiyo umefikia asilimia 64%, na
kwamba mradi huo unatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Julai mwaka huu.
Kwa upande wao Katibu wa Chama cha Mapinduzi CCM,
Sadick Kibwana Kadulo, pamoja na Meya wa Manispaa ya Kigoma Ujiji Musa Maulid,
wamesema meli hiyo ni mkombozi kwa wananchi wa Kigoma kwenye masuala ya usafiri
na uchumi.





Maoni
Chapisha Maoni