DC KIGOMA AWATAKA WANANCHI KULINDA MAZINGIRA KWA KUTUMIA NISHATI SAFI
![]() |
| FROLENCE MASUNGA MWAKILISHI ENVOTEC |
Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Dkt. Rashid Mohamed Chuachua, ametoa wito kwa wananchi wilayani humo kumuunga mkono Rais Samia Suluhu Hassan, kwenye ajenda ya matumizi ya nishati safi ya kupikia ili kulinda na kuhifadhi mazingira.
![]() |
| Rashid Chuchua Dc Kigoma |
Dkt. Chuachua ametoa wito huo wakati wa akizindua
ugawaji wa majiko sanifu ya kupikia ya gharama nafuu yenye ruzuku ya serikali,
kwa wananchi katika kata ya Simbo wilayani Kigoma, ambapo amesema kuwa matumizi
ya majiko sanifu ni hatua muhimu ya kubana matumizi na zaidi kulinda na
kuhifadhi mazingira, kwa kuwa majiko hayo yanatumia nishati kidogo.
Kampuni ya ENVOTEC iliyopewa dhamana ya kuuza majiko
hayo kwa bei ya ruzuku kupitia Wakala wa Nishati Vijijini REA, kwa ujumla
imegawa majiko 1,404 kwa wilaya ya Kigoma, ambapo mwakilishi wa kampuni hiyo
Florence Masunga, amesema wananchi watachangia asilimia 15% tu ya bei huku
serikali ikilipia asilimia 85%..
Baadhi ya wananchi waliopata majiko hayo akiwemo
Rehema Jackson, wameeleza furaha yao na namna watakavyoyatumia katika vijiji
vyao
Ikumbukwe kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Samia Suluhu Hassan ndiye kinara wa kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya
kupikia humu nchini na Afrika, kwa lengo la kulinda na kuhifadhi mazingira,
pamoja na kuwaepusha binadamu na madhara yatokanayo na matumizi ya kuni na
mkaa.







Maoni
Chapisha Maoni