KIBONDO YAENDELEZA KAMPENI KUUNGANISHA WATOTO WANAOISHI MITAANI NA FAAMILIA ZAO NA WENGINE KURUDISHWA MASHULENI
![]() |
| Aneth Kolman Mkuu wa Dawati la Jinsia Jeshi la Polis Kibondo |
![]() |
| Sophia Gwamagobe Afisa Ustawi wa Jamii Wilaya ya Kibondo Mkoani Kigoma |
![]() |
| Lukas Lazaro mwakilishi wa Mkurugenzi Halmashauri ya Kibondo |
![]() |
| Skola Kachiila Mkazi wa Kibondo |
![]() |
| Elias Jackson Mkazi wa Kibondo |
Kuendelea kuwepo Watoto wanaofanya kazi na kuishi
mitaani, hali hiyo imetajwa kuchochewa na baadhi ya Wazazi kutumia ukali zaidi
katika kuwakanya, migogoro ya familia, umasikini na utukutu wa watoto wenyewe
mambo hayo hupelekea kutoroka katika familia na kuishi mitaani
Wengi wa Watoto hao wanapoingia Mitaani huanza
kufanyabiashara za kuokota na kuuza chupa za plastic na Vyuma chakavu na
wengine kazi za majumbani na wanaokosa shughuli hujuhusisha na udokozi hatua
ambayo ni hatari kwa maisha yao maana wengi wao ni wanakuwa na umri mdogo
Hayo yamebainishwa katika maadhimisho ya Mtoto
anaeishi na kufanya kazi mitaani ambapo Afisa ustawi wa jamii wilaya ya Kibondo
Kigoma, Sophia Gwamagobe ameeleza kutokana hali hiyo watoto huroka majumbani
kuingia mitaani na kufanya kazihatarishi
Aneth Kolman
Mkuu wa Dawati la Jinsia Jeshi la Polisi Kibondo yeye amesistitiza umuhimu wa
wazazi kutimiza makujukumu ya malezi huku akiwataka Wadau kulitazama kundi hili
kwa jicho la pekeeili kuvinusuru vizazi vya vya sasa na vijavyo wengi wanakosa
masomo na maadili kwa ujumla
Maadhimisho yanalenga kujenga uelewa katika jamii ili
kupunguza wimbi la Watoto wanaoishi Mitaani jamii ikitakiwa kutambua suala zima
la majukumu ya malezi, huku Watoto wakitakiwa kuacha utukutu na kuwatii wazazi,
ameeleza hayo Lukas Lazaro akimwakilisha Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya
Kibondo katika maadhimisho hayo
‘’Nyinyi Watoto baadhi yenu mnajisababishia matatizo
kwasababu wengine mmetoroka katika familia bila sababu ila tu mliamua kujiunga
na makundi mkaanza tabia zisizo rafiki katika familia zenu na mnapoonywa
wengine mnataka kujidhulu kimwili, maana hata wazazi wanapowarekebisha, huo ni
upendo na uchungu kama wazazi wenu sasa nawashauri mjiepushe na tabia zisizofa
muwatii wazazi kwa mambo mema wanayo waelekeza’’ amesema Lukas
Elias Jackson na Skola Kachiila ni baadhi ya Wazazi
ambao wanaeleza kuwa hakuna mzazi anaefurahi Mtoto kuishi mitaani changamoto ni
utukutu wa Watoto na baadhi ya Wazazi kukwepa majukumu na kuomba sheria
zitumike kwani hali hiyo inaweza kuendeleza uwepo wa makumdi mabaya ya kiharifu
Pamoja na mambo mengine Wilaya ya Kibondo imeanza
kuondoa watoto hao mitaani na kuwaunganisha na familia zao na wale ambao
wameacha masomo wanarudishwa mashuleni na katika miezi miwili wameunganishwa
watoto nane katika familia, huku
ufutiliaji ukiendelea kutambua kila motto anakotokea







Maoni
Chapisha Maoni