KATIKA KUKABILIANA NA MAJANGA YA MOTO SERIKALI IMETOA GARI LENYE MTAMBO WA KUZIMIA MOTO KATIKA WILAYA YA KIBONDO
Wilaya ya Kibondo mkoani Kigoma imepokea gari (mtambo)
utakaosaidia katika kukabiliana na majanga ya moto yanapotoke
Uzinduzi wa mtambo umefanyika ofisi ya mkuu wa wilaya
ya Kibondo ambapo mkuu wa wilaya hiyo Kanali Aggrey Magwaza amesema mtambo huo
utasaidia kwa kiasi kikubwa hasa pale zitakapotokea changamoto za ajali za moto
Aidha ameagiza uongozi wa halmashauri chini ya
mwenyekiti wa halmashauri Bw. Alex Baragomwa kuhakikisha wanatoa ushirikiano
kwa zimamoto katika upatikanaji wa maji, mafuta na matengenezo ya mtambo huo
ili uendelee kutoa huduma katika hali ya ubora
Awali kaimu Kamada wa jeshi la zimamoto na uokoaji
mkoa wa Kigoma Mrakibu masaidizi Michale Maganga amesema imani yake ni kwamba,
kuwepo kw amtambo huo kutawafanya wananchi wa wilaya ya Kibondo wawe salama
zaidi dhidi ya majanga ya moto
Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Kibondo Bw.
Alex Baragomwa pamoja na mwenyekiti wa chama cha mapinduzi wa wilaya hiyo Bw.
Hamisi Tahiro wameomba elimu izidi kutolewa hasa katika kuepuka ujenzi holela
unaoweza kuepelekea kushindwa kufanyika kwa zoezi la kuzima moto kwa kukosa
mahali pa kupitisha mtambo huo.





Maoni
Chapisha Maoni