ONGEZEKO LA IDADI YA WATU NI TATIZO LA KIMATAIFA
Ongezeko la idadi ya watu Duniani, ni tatizo la kimataifa na na
linatajwa kusababisha changamoto mbalimbali za Kibinadamu japo uwepo wa
Binadamu katika uso wa Dunia ni jambo la muhimu
Kwa mujibu wa makadirio ya hivi karibuni ya Umoja wa Mataifa
kupitia Divisheni ya Idadi ya Watu ya UN (UN DESA Population Division), ni
kwamba kufikia mwezi Julai 2025, dunia
ilikadiriwa kuwa na zaidi ya watu bilioni 8.1.
Nchi zenye Idadikubwa ya Watu
Duniani ni ni China na India ambapo katika Nchi ya India kuna Watu wapatao
1,339,180,127 na China ikiwa na
Idadi ya Watu 1,409,517,397
huku Bara la Afrika likiwa na Watu billion 1.58
Kila uchao Wanadamu wamekuwa wakiongezeka kwa kasi huku Dunia ikiwa pale
pale na mahitaji ya lazima ya kibindamu
kama ardhi vikiwa haviongezeki na huduma za Afya, Maji, Chakula na makazi, upatikanaji wake ukiwa ngumu na kuufanya
ulimwengu kuwa katika hali ya hatari ya kukumbwa na Majanga ya Kibinadamu
Kutokana na hali hiyo, kila ifikapo Julai 11 kila mwaka Dunia uadhimisha
Siku ya Idadi ya Watu Duniani, lengo la kuadhimisha siku hii ni kuongeza uelewa kuhusu masuala
yanayohusiana na ongezeko la watu duniani, ikiwa ni pamoja na changamoto za
maendeleo endelevuili kwa ajili kuboresha upatikanaji wa huduma za Kijamii na matumizi
ya rasilimali na kuepuka athari za
kijamii na kimazingira
Maadhimisho haya hutumika pia kuhamasisha nchi wanachama
na mashirika mbalimbali kushirikiana katika kupanga sera zinazolenga kuboresha
maisha ya watu, hasa katika maeneo yenye ongezeko kubwa la idadi ya watu au
changamoto za kijamii na kiuchumi zinazotokana na idadi kubwa ya watu.
Tanzania kunakokadiriwa kuwa na zaidi ya
Watu zaidi ya Milion 61 licha ya
ongezeko la Idadi ya Watu, Elimu inahitajika kutunza Kilichopo kwa ajili ya
Vizazi vilivyopo na vijavo kama matumizi bora ya ardhi na utunzaji wa
miundombinu kama Vituo vya kutolea huduma za afya, Elimu Barabara Maji na
mingineyo mingi

Maoni
Chapisha Maoni