sera ya Taifa ya Wazee, haitekelezeki sababu haina sheria


Wazee wa umri wanatambuliwa kuwa ni moja raslimali  na nguvu mpya katika  maendeleo ya nchi hvyo wanatakiwa kupata fursa za kushiriki katika shuguli za  maendeleo sambamba na wananchi wengine  

Kulingana na hali ilivyo hivi sasa kwa sababu ya kuwepo kwa mmomonyoko wa maadili wazee katika jamii umewaathiri wazee walio wengi na kusababisha kukosa huduma mbalimbali stahiki hali inayopelekea kupoteza umuhimu wao 

Serikali ya tanzania ilifanya maamuzi ya kuwa na sera ya Taifa ya Wazee  mwaka 1999 ambayo ilitungwa mwaka 2003 kwa dhamira ya kuwasaidia kuondokana na changamoto mbambali  hatua ambayo imeokana kukwama katika utekelezaji wake kama  wanavyoongea katibu mtendaji Bi Clotrida Kokupima mwishoni mwa wiki iliyopita katika kikao kilichoandaliwa na chama cha wazee wilaya ya kasulu mkoani kigoma kwa kuwashirikisha waandishi wa habari

Bi Kokupima alieleza kuwa pamoja na mipango mingi ilimo ndani ya sera hiyo bado wazee wameendelea koukosa huduma kwasababu ya kukosekana kwasheria ya kuisimamia ser hiyo

Chama cha Wazee tawi la Kaslu kimeamua kuitisha kikao hicho na waandishi wa habari ili kujadili vikwazo vinavyowakabili na kuuhabarisha  umma  ijilikane kinachoendelea na kujenga weredi alisema mwenyekiti wa chama hicho Bw Chubwa Chubwa

Hata hivyo kaimu Mganga mkuu wa Hospitali ya wilaya ya Kasulu Bi Elina Kimaro amesema kuwa kwa kutambua hali hiyo waliamua kuweka dirisha kwa ajili ya kutoa huduma kwa Wazee japo yapo matatizo mengi yanayoikabili sekta ya Afya hasa kwa upande wa upatikanaji wa madawa

Kwa kuwa kikao hicho kiliwahusu waandishi wa habari na wazee hao, nao walilazimika kueleza ni namna gani wanavyofanyakazi juu ya maswala yanayowahusu wazee ambapo Dotto Elias toka Tbc 1 na  Muhingo Mwemezi wa Clouds Tv
Bi Clotrida Kokupima Katibu Mtendaji Swata Kasulu
Dotto Elias Tc Kigoma
Muhingo Mwemezi Clouds Tv Kigoma
Mwananchi na Richard Katunka wa Star tv, walieleza jinsi vyombo vyao vinavyofanya kazi na kuonyesha hali halisi ilivyo

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao