Risasi za SMG 599 zafukuliwa ardhini Kibondo

Baadhi  ya wakazi wa mji wa Kibondo mkoani Kigoma jana waliingia katika hali ya tahaluki baada ya mafundi ujenzi waliokuwa wakichimba msingi kwa maandalizi ya kujenga nyumba kufukua Lisasi za Bunduki aina ya SMG zipatazo 599 zinazoonekana kukaa muda mrefu ardhini.

Mmoja wa wakazi hao Bw, Jastin Samson alisema kuwa kama lisasi hizo zingeweza kuingizwa mitaani kwa kutumiwa na waalifu, kulikuwa na uwezekano wa kuumiza watu wengi

Lemijiusi Rabson ambaye alikuwa kibarua katika eneo la ujenzi lililoko katika mTaa wa Ihulilo Kata ya Kibondo mjini Wilayani hapa, amesema kuwa alipokuwa akiendelea na shuguli zake za kuchimba msingi kwa ajili ya maeendalizi ya ujenzi alifukua mkuko wa Sandalusi  uliokuwa umewekwa Lisasi ndani yake na kutaarifu kwa msimamizi wake aliyetoe na kuwaita Polisi

Msimamizi wa ujenzi huo, Bw, Jackson Amoni aliweka wazi  kuwa eneo hilo nila mtu mtu mmoja aliyefahamika kwa jina moja la Ally mkazi wa kibondo ,

Mweneyekiti wa Mtaa wa Ihulilo Nuhu Kasigwa ameeleza kuwa Eneo hilo lililokuwa likijengwa nyumba limekaa kwa muda mrefu sana bila kuwepo nyumba na kueleza kuwa kama hazikuwekwa na watanzania, uenda ziliwekwa na katika ujio wa Wakimbizi toka nchni Burundi kwani eneo hilo liko karibu maali walipokuwa wakipitia wakimbizi

Aidha  Kasigwa amewapongeza vijana hao waliokota lisasi hizo na kuamua kutoa taarifa Polisi ili taratibu husika zifuate maana kama wasinge kuwa wenye maadili mema wangeamua kukaa kimya na baadae zikatumika kuleta madhala katika jamii

Kijana Lemijiusi aliyefukua Rilsasi wakati akichimba msingi
Blog hii, ilifika katika ofisi ya mkuu wa wilaya kibondo ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wa wilaya, ili kufahamu zaidi na kukuta yuko safari, Katibu tawala hakupatikana kwa madai kuwa alikuwa na kikao nje ya ofisi huku Afisa Tarafa ya kibondo Moshi Hussein ambaye alibaki na ofisi alisema kuwa hawezi kuongea lolote kwani hajapata taarifa kutoka kwa mkuu wa polisi wa wilaya hiyo juu ya kuokotwa kwa Lisasi hizo
Mwisho


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao