Vijana raslimali muhimu katika nchi yoyote Duniani hivyo itumike vizuri




Vijana ni raslimali ya muhimu katika jamii na nchi yoyote Duniani hali inayowataka kujitambua kuwa wao ni watu wanaotegemewa kama nguvu nguvukazi Taifa hasa hapa Tanzania

Hayo  yaliwekwa wazi na Mwenyekiti wa uhamasishaji chama cha Mapinduzi wilaya ya Kibondo mkoani Kigoma Bw, Noberth Bulinjie wakati wa uchaguzi nafasi wa mbalimbali za umoja wa vijana wa Ccm [Uvccm] uliofanyika katika ukumbi wa Boma  wilayani humo
Bulinjie aliwataka vijana kujitabua vema kutokubali kurubuniwa na makundi ya aina yoyote au vyama vya siasa bali wanatakiwa kutumia nguvu zao walizonazo kwa wakati huu ili kuwa chachu ya maendeleo hapa nchini

Aidha alieleza kuwa wanasiasa wengi katika maeneo mengi Duniani upenda kuwatumia vijana ili kutimiza adhima yao hata kama wao hawajui kile wanachokipigania wala kuhoji ila kama vijana watajitambua umuhimu wao , uwezekano wa kushawishiwa kuingia katika matende ya uvunjifu wa Amani hautawezekana kwani wengi kwa kutofuata utaratibu uweza kupoteza maisha au kupata vilema vya kudumu

Nae Katibu wa uvccm Kibondo James Rafael aliwataka vijana wa umoja huo kutojiingiza katika makundi vya ulaji rushwa na matendo yasiyofaa katika jamii ili kuendeleza heshima ya chama hicho hasa wakati wa uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika octoba  mwaka huu Taarifa zaidi

Alieza kuwa nchi hii imekuwa na changamoto nyingi ikiwa pamoja na kukosa baadhi ya viongozi waadilifu ambao wamekuwa ni vikwazo katika kuwaletea maendeleo wananchi wao kutegemeana  na maeneo husika akitaja hatua kuwa hatua ambayo usababishwa na wananchi kufanya uchaguzi kwa kukomoa upande flani au kutumia jaziba  ushabiki na kuwaweka watu wasiofaa kwenye nyadhifa za kuwaatumikia watanzania na kuwaacha wakilalamika

Katika uchaguzi huo nafasi zilizokuwa zikipigania ni Katibu, Mjumbe wa mkutano mkuu wa mkoa,wajumbe wa kamati ya utekelezaji na Baraza la umoja wa vijana ccm ambapo waliopata nafasi hizo wote kuhakikisha wanafuata taratibu na kanuni umoja huo na chama kwa ujumla ili kuondokana na kukipaka matope na kupoteza Imani kwa wafuasi  na walio nje ya chama

 

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao