Membe: Nikiwa Rais Nyerere atafurahi

Lindi/Dar. Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Benard Membe, ametangaza rasmi nia ya kuutaka urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 2015 akisema anatosha na kwamba Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere huko aliko atafurahi endapo atakuwa rais.
Membe aliyasema hayo jana kwenye Viwanja vya Ofisi ya CCM Mkoa wa Lindi katika hotuba yake ya saa moja kutangaza nia yake hiyo huku kwa kujiamini kabisa akisema kuwa yeye ndiye Rais wa Tanzania kwa miaka 10 ijayo.
Alisema katika urais wake, ataboresha elimu, ataweka msisitizo katika utawala bora, maendeleo ya jamii, uchumi na masuala mbalimbali ya kisiasa na kidiplomasia.
Huku akishangiliwa na maelfu ya watu waliofika kumsikiliza, alisema amejipima na kuona anaweza.
“Nimetafakari sana, nimeona ninatosha kwa nafasi hii nyeti…, nafasi adhimu na si ya mzaha japo naona wapo wanaofanya mzaha. Nimeangalia nikaona hakuna mwingine wa kufanana na mimi.
“Sikukurupuka, zipo nafasi za kukurupuka na wapo wanaokurupuka, lakini si vyema kukurupuka kwa nafasi ya urais,” alisema.
Membe aliyesindikizwa na mkewe Dorcas, alisema Machi mwaka huu alikwenda Butiama na kuzuru kaburi la Mwalimu na kupiga goti na kumweleza nia yake ya kuutaka urais.
“Nilipiga goti nikamwambia Mwalimu, navitaka viatu vyako, alivivaa Mzee Mwinyi (Ali Hassan), Mzee Mkapa (Benjamin) na Kikwete (Jakaya), sasa nataka kuvaa mimi na nina hakika vinanitosha.
“Ninaamini vitanitosha. Nikamwambia chondechonde, kama havitanitosha, niambie… timu yangu ya mikoani ikawahi kuniambia unatosha,” alisema Membe.
Alisema alialikwa na Mzee Mwinyi katika ‘birthday’ yake ya miaka 91 na kati ya mambo aliyomwambia ni kwamba ameongoza nafasi mbalimbali, lakini hakuwahi kununua uongozi.
“Mzee Mwinyi aliniambia kuwa alipata vyeo bila kununua, alisema sikuwa na magunia ya pesa miee…, sikununua wajumbe. Sasa, utajisikiaje kununua vyeo? Utawaangalia kwa jicho gani wanapokosea na utachukua hatua gani kuwawajibisha? Kuna vitu vya kununua laki
ni si Ikulu. Ikulu hainunuliki.”

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao