Viongozi wanaoaminiwa na kupewa dhamana ya kuwaongoza wananchi wametakiwa kujijengea mazingira ya uaminifu kwa kutenda yale yanayostaili na kuenenda kwa kufuata sheria taratibu na kutimiza viapo vyao ili kuondoa kukata tamaa kwa wananchi wao

Viongozi wanaoaminiwa na kupewa dhamana ya kuwaongoza wananchi wametakiwa  kujijengea mazingira ya uaminifu kwa kutenda yale yanayostaili na kuenenda kwa kufuata sheria  taratibu na kutimiza viapo vyao ili kuondoa kukata tamaa kwa wananchi wao
Erick Marey Hakimu wa wilaya ya Kibondo wakati wa kuwahapisha madiwani Halmashauri ya Kakonko
Peter Toyima Dc Kakonko

Akizungumza juzi, katika uzinzinduzi wa Baraza la Halmashauri la walaya ya Kakonko Mkoani Kigoma,  Hakimu wa Mahakama ya wilaya ya Kibondo Erick Marey wakati wa kuwahapisha madiwani alisema kuwa kiapo ni ishara ya utii kwa mlengwa hivo ni lazaima kifuatwe kwa kuyatenda yale kwa mujibu wa sheria na taratibu za nchi na kinyume na hasipofuata taratibu hizo anastaili kufikishwa katika vyombo vya sheria ili kuwajibishwa


Katika kikao hicho mara baada ya kuhapishwa madiwani hao, ulifanyika uchaguzi wa mwenyekiti  wa halmashauri na makamu wake ambapo Juma Maganga kata ya kakonko, alipata kura 12  huku mpizani wake Eliya Kanjero kata ya Gwarama, Chadema akiibuka na kura 10 kati ya  22 zilizopigwa, hivyo Juma Maganga kutangazwa mshindi na kisha  kuomba ushirikiano na wananchi katika utendaji kazi

Maganga aliwataka madiwani wenzake kuahakikisha wanaondoa itikadi zao za kisiasa na kushirikiana kwa kufanya kazi na kudai kuwa hatakuwa tayari kuona migawanyiko kati yao inaendelea na watakiwa kushirikiana na si kuharibiana kazi maana kauli mbiu ya serikali ya sasa ni kuwajibika  


Kwa upande wa  nafasi ya makamu mwenyekiti  Bw, Toyi Slivester  wa kata ya Gwanumpu, ccm alipata kura 12 dhidi ya mpinzani wake Bw, Nobert Gwimo Chadema, akipata kura 10 na baadae katibu tawara wa wilaya hiyo Zainabu Mbunda, kumtangaza Toyi Slivester, kuwa mshindi wa nafasi hiyo..


Hata hivyo baadhi wakazi  wa Kakonko waliohudhulia kwenye kikao hicho ambao ni Ashura Mbopewe na Angelina Baraka waliwataka viongozi hao ikiwa ni Mbunge na Madiwani kuhakikisha wanayatimiza yale waliyoyaahidi kwa wananchi wakati wa Kampeni hasa katika maeneo ya vijijini kwa wanakabiliana na changamoto nyingi kama elimu duni, Maji,  Barabara ukosefu wa Pembejeo za kilimo


Kwa upande wake Peter Toyma ambaye ni mkuu wa wilaya hiyo aliwataka madiwani hao kuachana na mambo yaliyopita katika kampen za uchaguzi na kushikama katika utendaji kazi ili kuleta maendeleo na kusema kuwa serikali haitamvumilia yeyote atakayeenda kinyume na maelekezo

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao