Wastaafu wa kada mbalimbali hapa nchini wametakiwa kuwa chachu ya maenedeleo kwa kuwasadia wale walioko makazini kwa kutoa ushauri juu ya vikwazo walivyo kutana navyo kazini ikiwamo, na mafanikio kwa ujumlana namna ya kufanya kazi kwa welediNdyaki Majo katibu cwt Kibondo

Wastaafu wa kada mbalimbali hapa nchini wametakiwa kuwa chachu ya maenedeleo kwa kuwasadia wale walioko makazini kwa kutoa ushauri juu ya vikwazo walivyo kutana navyo kazini ikiwamo, na mafanikio kwa ujumlana namna ya kufanya kazi kwa weledi

Wito huwo  umetolewa na Katibu wa chama cha walimu wilaya kibondo Bw,Ndyaki Majo wakati wa hafra fupi ya kuwaaga walimu wastaafu iliyofanyika kwenye ukumbi wa chama hicho mjini kibondo.

Majo amesema kuwa hivi sasa taaluma ya ualimu imejumuisha vijana  wengi ambao wanapangiwa kufanya kazi katika maeneo mengi ambao wanahitaji maelekezo waweze kupata ufanisi katika utendaji kazi hivyo, kama ni kustaafu ni kwa mujibu wa taratibu tu  lakini mchango wao bado unahitajika

Nae mwenyekiti wa chama hicho wilaya ya kibondo Tilimio Nzigo, amesema kuwa lengo la kutoa mkono wa kwaheri kwa wastaafu, ni kutambua  mchango wao walioutoa kwa umma, na kuongeza kuwa chama kinatambua kuwapo kwa changamoto zinazoendelea kuwakabili walimu na kitaendelea kuishauri serikali iweze kuzitatua


Kwa upande wao baadhi ya wastaafu ambao ni Pantaleo Bilikundi na Simon Magoti waliwataka wanaoabaki makazini kufanya kazi kwa umakini wakijua kuwa taaluma ya ualimu inategemewa sana, na kujijengea tabia ya kuacha kugoma mara yanapotokea matatizo kwa kufanya hivyo ,ni kuwaadhibu wanafunzi wasiyokuwa na hatia


Walimu walioagwa kila mmoja alipewa mkono wa kwaheri kwa kupatiwa bati zenye thamani ya Tsh 320,000/ ambapo  wote sita jumla ni 192,000/    


Walimu wastaafu wakiwa katika moja ya kukabidhiwa zawadi cwt mjini Kibondo


Majo Ndyaki  katibu cwt Kibondo

Pantaleo Bilikundi Mstaafu

Baadhi ya wastaafu

Mwenyekiti wa chama cha walimu kibondo Tilimio Nzigo, akimkabidhi zawadi mmoja wa wastaafu Simon Magoti
Tilimio Nzigo mwenyekiti Cwt Kibondo

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao