Ili kuweza kuondoa kero ya umeme kwa wananchi wa Mkoa wa Kigoma na kuhepusha garama kubwa katika uzalishaji wa Nishati hiyo Shirika la umeme Tanesco lina mpango wa kuanzisha mradi wa kuzalisha umeme kwenye Mto Malagarasi kwa kuokoa garama kubwa za uendeshaji


Medard Kaleman Naibu waziri Nisahati Madini


Ili kuweza kuondoa kero ya umeme kwa wananchi wa Mkoa wa Kigoma na kuhepusha garama kubwa katika uzalishaji wa Nishati hiyo Shirika la umeme Tanesco lina mpango wa kuanzisha mradi wa kuzalisha umeme kwenye Mto Malagarasi kwa kuokoa garama kubwa za uendeshaji.
Sababu inayochangia garama kuwa kubwa ni mitambo ya kuzalisha umeme iliyoko katika wilaya zote za mkoa huo inatumia mafuta ambayo ununuliwa kwa kiasi kikubwa hku wateja wa umeme wakiwa ni wachache huku shirika hilo likifanya kazi kwa hasara  

Akiongea na waandishi wa habari,  Naibu waziri wa Nishati na Madini Dkt Medard Kalemani alipokuwa wilayani  juzi Febr 20 wilayani Kibondo  wakati wa ziara ya kikazi na kutembelea miradi ya umeme mkoani humo ambapo, amesema kuwa shirika la umeme Tanesco katika Mkoa wa Kigoma linatumia shilingi million 60 kwa siku moja hatua ambayo ni hasara ikilinganishwa na idadi ndogo ya wateja wa nishati hiyo

Kalemani alisema kuwa mradi wa malagaras ulikuwa uanze kutekelezwa mwaka 2009 katika eneo la Igamba 2 ila baada ya kugundulika kuwa eneo hilo kuna vyura na konokono ambao hawapatikani Duniani na  mujibu wa sheria za mazingira za umoja wa mataifa ukaahirishwa ila sasa mradi huo utatekelezwa julay 2016 eneo la Igamba 3 ili kuweza kuwapatia wananchi umeme wa uhakika
Awali akitoa taarifa ya wilaya kwa Naibu waziri huyo, mkuu wa wailaya ya Kibondo Bi, Ruth 

Msafiri alisema  kuwa tatizo kubwa kwa watu wanaochukua Kandarasi za kufunga umeme wa Rea kuchelewa kukamilisha kazi zao hali inayo sababisha malalamiko kwa wananchi na kutoleta usawa katika jamii,huku naibu waziri huyo akieleza kuwa wato waliopewa kandarasi za ujenzi wa miundo mbinu kupitia Rea, wamepewa muda ifikapo julay mwaka huu, wawe wamekamilisha kila kitu yabaki matatizo madodomado

Sambamba na hilo, mwenyekiti wa Simon Kanguye, ambaye ni mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya hiyo, alimuomba kushugulikia swala la ufungaji wa umeme katika Taasisi mbalimbali ikiwa ni Zahati, Vituo vya Afya,Polis na shule za sekondari ambazo zina maabara kwa ajili ya kujifunzia sayansi na uendeshwaji wake unaitaji  Nishati ya umeme bila hivyo hazitakuwa na kazi

Kwa upande wao baadhi ya wananchi wameiomba serikali kupitia shirika hilo kupunguza garama za umeme ili  hata mwenye uwezo wa chini aweze kumudu garama hizo kwa kutumia umemekama alivyosema Chikola Staphord mkazi wa Kibondo
Mwisho


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao