Wadau mbalimbali wilayani kibondo mkoani kigoma wakiongozana na mkuu wa wilaya hiyo Bi.Ruthi Msafiri wametoa vitu mbalimba katika shule ya msingi nengo ya watoto wenye ulemavu vyenye thamani ya shilingi laki nne na nusu ili kutia hamasa kwa watoto kujisomea kwa uhuru.


Ruth Msafiri Dc Kibondo akiwa na baadhi ya watoto walemavushuleni Nengo


Nashon Amosi mwalimu katika shule ya msingi Elimu maalum Nengo Kibondo

Ally Kombe katibu Jumhiya ya wazazi ccm W Kibondo

Wadau mbalimbali wilayani kibondo mkoani kigoma wakiongozana na mkuu wa wilaya hiyo Bi.Ruthi Msafiri  wametoa vitu mbalimba katika shule ya msingi  nengo  ya  watoto wenye ulemavu vyenye thamani ya shilingi laki nne na nusu ili kutia hamasa kwa watoto kujisomea kwa uhuru.

Akizungumza na wazazi na walezi  katibu wa jumuia ya wazazi ccm  wilayani hapo Bw.Ally Gombe amesema hatua ya kupeleka zawadi hizo  ni baada ya kuona watoto hao wakipata adha mbalimbali wawapo shuleni na hivyo kuona umuhimu wa kuwatembelea katika njia ya kutambua haki za watoto.

Amesema jamii haina budi kuwa na mazoea ya kuwatembelea watoto hao mara kwa mara ili kuweza kuwafariji pamoja na kuwapa zawadi mbalimbali ambazo zitawahamasisha kusoma kwa bidii kuwafanya jisikie kuwa nao ni miongoni mwa  wanajamii.

Akitoa shukrani zake mkuu wa shule hiyo Shaban Mzenze amepongeza uamuzi huo,nakueleza kuwa inatia faraja kwa watoto hao wanapotembelewa na watu tofauti kulingana hali zao za ulemavu maana wote wanashinda  ndani uzio muda wote

Sambamba na hilo, baadhi ya walimu wamesema kuwa kwa hivi sasa wanafunzi hao wanaishi katika mazingira ambayo si rafiki wakikakabiliana na vikwazo vya kukosa vifaa maalum vya kujifunzia hasa kwa walemavu wa macho, shule kukosa njia maalum za kupitia walemavu kwani walemavu wa viungo ushindwa kufika eneo la kuchukulia chakula kwani mvua ikinyesha eneo lote ujaa tope

Nae mkuu wa wilaya ya kibondo Ruthi Msafiri akizungumza na wazazi na walimuamewataka walimu kuwa wavumilivu wakati serikali ikifanya taratibu za kuboresha huduma za elimu

Shule hiyo ya Nengo elimu maalum inahudumia watoto walemavu wa aina mbalimbali ikiwa ni pamoja na utindio wa ubongo walemavu wa Ngozi,Wasiyoona, na walemavu wa viungo

Maoni

  1. Nakupongeza sana kaka kwa jitihada zako za kutuza mambo yanavyoendelea

    JibuFuta

Chapisha Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao