Walengwa wa Mpango wa Kunusuru kaya Masikini Wilayani Kibondo Mkoani Kigoma walipo katika mpango huo wengi wanashindwa kufika katika vituo vya ugawaji wa fedha jambo ambalo huchangia baadhi ya kaya kuzikosa fedha hizo zenye lengo la kuzisaidia kaya masikini kupata mahitaji muhimu.


Walengwa wa Mpango wa Kunusuru kaya Masikini Wilayani Kibondo Mkoani Kigoma walipo katika mpango huo wengi wanashindwa kufika katika vituo vya ugawaji wa fedha jambo ambalo huchangia baadhi ya kaya kuzikosa fedha hizo  zenye lengo la kuzisaidia kaya masikini kupata mahitaji muhimu.

ilibainika walengwa wa mpango huo walio hama vijijini kwao na kwende kuanzisha mashamba mapya pembeni mwa Hifadhi ya Wanyama pori Moyowosi Kigosi na Vijiji vya Kumubanga na Kumuhasha wanashindwa kufika zoezi la ugawaji wa fedha kutokana na kukosa taarifa za ugawaji fedha.

Jumla ya kaya 119 hazikuweza kupata fedha za uhawilishaji kwa awamu ya  tatu kutokana na uendeshaji wa shughuli za kilimo mbali na makazi ya  watu ambapo wengine 11 wamefariki dunia  hali ambayo inachangia kuwepo kwa malalamiko katika zoezi hilo.

Mwenyekiti wa Kamati ya ugawaji fedha katika Kijiji cha Kisogwe kata Busunzu Bw.Yona Emmanuel Amesema Changamoto ya walengwa kuto jitokeza siku ya ugawaji wa fedha hali  hiyo imechangia kaya lengwa kukwamisha mpango wa maendeeo ya serikali kwa kupunguza tatizo la kumasikini wa familia na kuboresha hali ya upatikanaji wa chakula bora kwa watoto, kupunguza utoro mashuleni na kuboresha hali ya upatinaji wa huduma ya afya kwa watoto.

Alisema tatizo la kijografia limechangia walengwa kushindwa kupata taarifa ya siku ya ugawaji wa fedha kwa kaya masikini katika vijiji husika na hivyo kupelekea walengwa wengi kutopata haki yao. 

“changamato kama hii ilijitokeza hata wakati wa zoezi la undikishaji na utambuzi wa kaya masikili jambo ambalo kaya nyingi zinakosa haki zao kutokana na kuhama hama”.

Naye Afisa Mtendaji wa kata ya Busunzu Bi.Agenes Josephat amekili kuwepo kwa tatizo hilo na kwamba licha ya jukumu lao la kutoa taarifa kwa wananchi juu ya zoezi la ugawaji wa fedha za uhawilishaji kwa kaya masikini lakini wanapata wakati mgumu wa kifikisha taarifa hizo kutokana na jografia pamoja na kutoakuwa na taarifa ni wapi walengwa wamehamia kwaajili ya shughuli zao za kilimo.

Kwa upande wake Mratibu wa TASAF Wilaya ya Kibondo Bw. Hassan Nkuro amekili kuwepo kwa changamoto hiyo na kukili kuwa katika zoezi la ugawaji wa fedha awamu ya tatu katika kipindi cha January na February 2016 walegwa 119 hawakupata fedha zao kutoka  na kutofika katika vituo vya ugawaji wa fedha.

Alisema Wilaya ya Kibondo inajumla ya  walegwa wa kaya masikini 10,254 kutoka katika Vijiji 40 vilivyopo katika kata 13 za Wilaya hiyo ambapo fedha zilizolipwa kwa walengwa ni shilingi  Milioni 348,960,000  na kiasi kilicho rudishwa ofisi ya TASAF makao makuu kutokana na walengwa kutofika katika vituo vya ugawaji wa fedha hizo ni shilingi 3,440,000.

Hata hivyo Mratibu huyo ameisisitiza jamii kuzingatia masharti na maelekezo katika matumizi ya fedha hizo  kwa kuwa nunulia wanafunzi sare za shule na madafri, kupeleka watoto krini na kuwapatia chakula bora pamoja na kuanzisha shughuli ndogondogo za kukuza kipato kama kufunga mbuzi na kuku wakatakao wasaidia ba

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao