Korea Kusini imetoa ombi la kutaka kufanyika mazungumo ya juu na Korea Kasuni tarehe 9 mwezi huu kujadili ikiwa kuna uwezekano wa kushiriki mashindano ya masimu wa baridi mwaka 2018. Hii ni baada ya kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un kusema kuwa alikuwa anatafikiria kutuma timu kwenda Pyeongchang nchini Korea Kusini kwa mashindano hayo mwezi Januari.

Ni wanariadha wawili tu wa Korea Kaskazini waliofuzu kwa mashindano ya mwaka huu ya msimu wa baridi nchini Korea Kusini

Kim Jong-un alisema kuwa alikuwa anatafikiria kutuma timu kwenda Pyeongchang nchini Korea Kusini kwa mashindano hayo mwezi Januari.
Korea Kusini imetoa ombi la kutaka kufanyika mazungumo ya juu na Korea Kasuni tarehe 9 mwezi huu kujadili ikiwa kuna uwezekano wa kushiriki mashindano ya masimu wa baridi mwaka 2018.
Hii ni baada ya kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un kusema kuwa alikuwa anatafikiria kutuma timu kwenda Pyeongchang nchini Korea Kusini kwa mashindano hayo mwezi Januari.
Alisema kuwa nchi hizo mbili zinahitaji kukutana kwa dharura kuzungmzia uwezekano wa kushiriki mashindano hayo.
Mapema rais wa Korea Kusini alisema kuwa ameiona hiyo kama fursa ya kuboresha uhusiano ulioharibika kati ya nchi hizo.

Waziri wa mapatano wa Korea Kusini Cho Myoung-gyon alipendekeza Jumanne kuwa wawakilishi watakutana katika kijiji ya mapatano cha Panmunjon.
Kijiji hicho kilicho eneo lenye ulinzi mkali la DMZ mpakani ndipo mazungumzo kati ya nchi hizo yamekuwa yakifanyika.
Bado haujulikani ni nani atahudhuria mazungumzo hayo ya tarehe tisa Januari, na Korea Kaskazinia bado haijajibu.
Mazungumzo ya mwsiho ya juu yalifanyika Disemba mwaka 2015 katika eneo la pamoja la viwanda la Kaesong.
Yalimalizika bila makubaliano yoyote na ajenga ya mazungumzo haikutangazwa.
CHANZO CHA HABARI HII NI BBC

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao