Serikali imesema inalenga ifikapo mwaka 2021 vijiji vyote hapa nchini vitakuwa visambaziwa nishati ya umeme ili kuondoa changamotombalimbali zinazowakabili wananchi ikiwa ni pamoja na kukuza uchumi hasa katika maeneo ya Vijijini



 Muhingo Mwemezi



Medad Kaleman Waziri wa Nishati na Madini

Raymon Seya [Tanesco]

Bangie Msofe[Rea]




Kibondo

Serikali imesema inalenga ifikapo mwaka 2021 vijiji vyote hapa nchini vitakuwa visambaziwa nishati ya umeme ili kuondoa changamotombalimbali zinazowakabili wananchi ikiwa ni pamoja na kukuza uchumi hasa katika maeneo ya Vijijini

Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Nishati na Madini Medadi Kalemani wakati wa uzindizi wa Rea awamu ya tatu uliofanyika kimkoa katikata ya mabamba wilayani kibondo mkoani Kigoma ambapo amesema hadi hivi sasa vijiji vilivyobaki ni 7873 Nchi nzima

Aidha Kalemani amewataka Watanzania kutokana na  hatua hiyo ya serikali kupitia wizara ya Nishati na Madini kuchangamkia fulsa hiyo kwa kuboresha miundo mbinu majumbani ili waweze kupata huduma hiyo muhimu

Katika Uzinduzi huo mkuu wa Mkoa Kigoma Brigedia General Mstaafu Emmanuel Maganga amemtaka Mkandarasi kufuata taratibu za makubaliano  na kuwataka wakuu wa wilaya za mkoa huo kuhakikisha wanafuatilia hatua zote na mkandarasi anavyofanya kazi


Kwa upande wake  mwakilishi wa Mkurugenzi wa huduma za Kiufundi wa Taasisi ya wakala wa huduma za umeme Vijiji Rea, Bengie Msofe, amesema atahakikisha kazi zina kwenda kama zilivyopangwa na kuwaomba wananchi ushirikiano huku mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu Tanesco   Raymond Seya, akisema kuwa watazingatia viwango  vya ubora wa mradi kama inavyotakiwa na wanakamilisha kwa wakati


Mradi wa ujenzi wa miundo mbinu ya umeme katika wilaya za Kakonko na Kibondo ni wa thamani ya shilingi billion 25 fedha za kitanzania na mkoa mzima mzima wa kigoma, thamani yake ni shilingi billion 60 hadi kukamilika
 Mwisho

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao