Rouhani amjibu Trump na kusema ni adui wa Iran

Mamlaka za Israel zimemfungulia mashtaka msichana mpalestina ambaye alirekodiwa kwenye video akimshambulia mwanajeshi wa Israel.
Ahed Tamimi, 17, na binamu yake walirekodiwa kwenye video wakiwakabili wanajeshi wa Israel katika kanda iliyosambaa pakubwa katika mitandao ya kijamii.
Anakabiliwa na kesi 12 ikiwemo dhuluma na kurusha mawe.
Lakini familia yake inasema kuwa walihusika kwenye maandamano katika eneo linalokaliwa na Israel la Ukingo wa Magharibi.
Jeshi la Israel linasema kuwa wanajeshi hao walikuwa wakiwazuia wapalestina kutokana na kurusha mawe kwa waendesha magari.
Video hiyo iyorekodiwa tarehe 15 Disemba ilionyesha kikundi cha wanawake akiwemo Tamini, wakiwapiga wanajeshi wawili wa Israel waliokuwa wamejihami vikali.
Ilisambaa sana katika mitandao na wapalestina wengi wamemsifu Tamini kuwa shujaa kwa kuipinga Israel.
Ahed Tamimi, 17, na binamu yake walirekodiwa kwenye video wakiwakabili wanajeshi wa Israel

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Shule ya msingi Nengo ya Walemavu, iliyoko wilayani Kibondo mkoani kigoma, inayohudumia wanafunzi walemavu wa mahitaji maalum inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwa ni ukosefu wa maji Vifaa vya kujinfunza na kufundishia na vyombo vya kulia chakula