KIBONDO YAENDELEZA UDHIBITI UGONJWA EBOLA
![]() |
| DktSimon Omary Mratibu huduma za Afya Wilaya ya Kibondo |
![]() |
| Fiboreen Siwale Mratibu wa Maralia Wilaya ya Kibondo |
![]() |
| Aggrey Magwaza Mkuu wa Wilaya ya Kibondo |
Mkuu wa wilaya ya kibondo Mkoani Kigoma, kanali Mstaafu Agery Magwaza amewaagiza wataalamu wa afya
kuendelea kufanya tafiti za kudhibiti maambukizi ya ugonjwa wa maralia kutokana
na ugonjwa huo kutodhibitiwa kwa ufasaha na kuendelea kuleta athari kwa jamii
Amebainisha hayo wakati wa kikao Cha kamati ya afya ya
msingi ya Wilaya, walipokua wakijadili namna ya kudhibiti ugonjwa huo ambapo
amesema maambukizi ya ugonjwa yamekua yakisababisha madhara kwa jamii kutokana
na mbu wannasambaza vimelea hivyo vya malaria kushidwa kudhibitiwa ipasavyo
Aidha katika
kikao hicho kilijadili namna ya kukabiliana na ugonjwa wa ebola ndani ya wilaya
ya kibondo huku mkuu huyo wa wilaya akwahimiza wananchi kuendelea kuchukua
tahadhari dhidi ya ugonjwa huo ikizingatiwa Wilaya hiyo iko mpakani mwa nchi, Ili usienee ndani ya wilaya ya kibondo na
kuweka maandalizi ya kukabiliana na ugonjwa wa ebola
Nao baadhi
ya wajumbe walioshiriki katika kikao hicho Vedasto Pesambili na Hamisi Tahilo,
wameomba elimu zaidi iendelee kutolewa kwa wananchi kuhusiana namna ya
kupambana na ugonjwa huo Ili uweze kudhibitiwa
Akiwasilisha
taarifa mbele ya kamati hiyo mratibu wa maralia wilaya ya kibondo Fibinoreen
siwale amesema wameendelea kuchua hatua mbalimbali za kuudhibiti ugonjwa huo
Ili kuweza kuutokomeza ndani ya wilaya ya kibondo
Kwa upande wake msimamizi wa huduma za afya
wilaya ya kibondo dokta Saimoni Omary amesema kama wilaya wamekwisha jipanga
vizuri kwaajili ya kukabiliana na ugonjwa wa ebola ndani ya wilaya Ili kuweza
kuakbiliana na ugonjwa huo wakati utakapo tokea





Maoni
Chapisha Maoni