UWINDAJI HARAMU WASABABISHA IDADI SOKWE KUPUNGUA GOMBE
Na Emmanuel Matinde Kigoma
Idadi
ya wanyama aina ya Sokwe katika Hifadhi ya Taifa ya Gombe iliyoko mkoani
Kigoma, inaelezwa kupungua kwa kasi kutokana na kuwindwa, kuharibu maeneo
yao ya asili, pamoja na shughuli za kibinadamu ambazo zinahatarisha maisha
yao.
Hayo
yameelezwa na Mkurugenzi wa Utafiti wa Sokwe kutoka Taasisi ya JANEGOODALL
(JGI), Dr. Deus Mjungu, huku akitoa wito kwa wadau wote kuona umuhimu wa
kuwalinda Sokwe ili waweze kuongezeka.
Nchini
Tanzania Sokwe, hupatikana katika mikoa ya Kigoma, Rukwa na Katavi lakini
kuongezeka kwa idadi ya watu na katika maeneo yaliyo karibu na makazi yao
kunatajwa kutishia maisha yao amesema ShedrackKamenya Mhifadhi Mkuu Mstaafu
toka Taasisi ya JGI.
Ikumbukwe
kuwa wanyama aina ya Sokwe ambao tabia zake hufanana kwa asilimia 98% na
binadamu, ni kivutio cha utalii kinachoiingizia serikali fedha za kigeni na
kusaidia kukuza uchumi hivyo jamii ina jukumu la kushirikiana na serikali
kuhakikisha wanaendelea kuishi.
.




Maoni
Chapisha Maoni