SIKU YA UJUZI KWA VIJANA










Monica Mwita Mwanafunzi Veta Mwanza


Voronica Gabriel Mkufunzi Veta Mwanza




Flaviana Minda Kaimu Mkuu wa Chuo Veta Mwanza



 

 Yapo naneno ya Wahenga yasemayo,Ushindi ni Mwenendo, Mwenendo huo ni Kazi, Kazi ni mawazo, mawazo ni kuelewa na imani, na hivyo kila kitu kinaanzia kwa  binadamu.

Kuendana na maneno hayo,mnamo  2014, Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa lilitangaza tarehe ya Julai 15 iwe siku ya Ujuzi wa Vijana Duniani, kuweka mikakati ya kuwaandaa vijana kwa ujuzi unaohitajiwa kuwaajiri na kuwawezesha kupata kazi licha ya kuwawezesha kwa Ujasiriamali. 

 

Siku ya Kimataifa ya Ujuzi kwa Vijana huadhimishwa kila tarehe 15 Julai. Siku hii ilianzishwa na Umoja wa Mataifa ili kuhamasisha na kutambua umuhimu wa kuwapa vijana ujuzi na stadi mbalimbali za kazi ili waweze kujitegemea kimaisha na kuchangia maendeleo.

Lengo kubwa ni kukumbusha jamii na serikali kutoa nafasi za mafunzo zitakazowawezesha vijana kupata ujuzi unaohitajika katika soko la ajira, hasa katika ulimwengu wa sasa wa kidijitali. Veta Mwanza ni moja ya Taasisi inayomilikiwa na Mamlaka za vyuo vya Ufundi Stadi imekuwa ikitoa maarifa ya Ujuzi Taaluma mbalimbali kama ususi Ushonaji Ufundi Magar,  Bomba, Upakaji rangi na nyinginezo

Baadhi ya Wanafunzi wanaopata ujuzi katika chuo hicho ambao ni Nuru Samweli na Hapnes Modest wamesema maarifa wanayoyapata katika chuo hicho yamekuwa yakiwafungua kifikra na kubadilisha mitazamo licha ya kupata ujuzi

Veronika Gabriel ni Mkufunzi katika fani ya ushonaji yeye anaeleza kuwa mafunzo yanayotolwa katika chuo hicho yanamwezesha Kijana kushindana katikasoko la ajira

Aidha Wanafunzi wengine  wameeleza kuwa Vijana wasiokuwa na taaluma wanapata Changamoto nyingi katika kuendesha maisha yao ndiyo sababu wao  kutafuta ujuzi maarifa wamebainisha Monica Mwita na Yohana Maguta wanafunzi wanaopata ujuzi wa uunganishaji wa vyumba kwa uchomeleaji

‘’Kwa kawaida sehemu zote wanahitaji mafundi hivyo bila ujuzi ajira lazima liwe tatitazo na sasa popote utakapokwenda kuhitaji kupata namna ya kutumikia Watu lazima uwe na ujuzi si maneo hivyo ujuzi ni lazima kwa kila mmoja’’ amesema Yohana

Kwa upandewake  Kaimu Mkuu wa Chuo cha Ufundi Veta  Mwanza Flaviana Minda ameeza kuwa wamekuwa wakijitahidi kuhakikisha wanaitikia wito wa serikali kuwapatia Vijana ujuzi  ambao unawasaidia kukabiliana na Changamoto za maisha

‘’Mazao yanayotoka katika chuo hiki, ni bora zaidi na yanafaa katika Sekta husika hivyo Vijana wote wenye uhitaji wa ujuzi wowote kulingana na kila mmoja anavyojitambua na mahitaji yake yalivyo, wanakaribishwa’’ amesema Flaviana

 

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

KATIKA KUKABILIANA NA MAJANGA YA MOTO SERIKALI IMETOA GARI LENYE MTAMBO WA KUZIMIA MOTO KATIKA WILAYA YA KIBONDO