Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia 2016

Kibondo;Mkuu wa wilaya ya Kibondo mkoani kigoma Luis Bura amemwagiza mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya hiyo kuwasimamisha kazi watumishi 3 wa idara ya ujenzi kutokana na ubadhilifu wa fedha za ujenzi wa vyumba vya madarasa na nyumba ya walimu katika shule ya sekondari Itaba

Picha
Kibondo; Mkuu wa wilaya ya Kibondo mkoani kigoma Luis Bura amemwagiza mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya hiyo kuwasimamisha kazi watumishi 3 wa idara ya ujenzi kutokana na ubadhilifu wa fedha za ujenzi wa vyumba vya madarasa na nyumba ya walimu katika shule ya sekondari Itaba Watumisha hao wanatuhumiwa kudanganya ili mkandarasi anaejenga nyumba hizo kulipwa milion 109 malipo ya wamu ya pili kwa madai kuwa ujenzi umekemilika kwa asilimi 85% ambapo milion 46 zimelipwa bila kufanyiwa kazi yoyote huku ujenzi ukiwa chini ya viwango na ukiwa uko chini ya asilimia 50% kama alivyoeleza mkurugenzi wa halmashauri hiyo Juma Mlehe kwa waandishi wa habari na wananchi Mkuu huyo wa wilaya katika maelezo yake alisesema matatizo ya ubadhilifu wa fedha za serikali katika wilaya hiyo yamekuwa ni mambo ya kawaida huku akilalamikia makundi ya wanasiasa kuingilia shughuli za kitaalam kwa kuwalazimisha watumishi wa halmashauri kufanya  mambo wanayoyataka wao  na kuwataka kufu

Mgombea wa urais wa Marekani kwa tikiti ya chama cha Republican Donald Trump ameimarisha kampeini zake mjini Nevada licha ya kisa cha usalama kilochobabisha walinzi wake kumuondoa jukwaani kwa muda.

Picha
Mgombea wa urais wa Marekani kwa tikiti ya chama cha Republican Donald Trump ameimarisha kampeini zake mjini Nevada licha ya kisa cha usalama kilochobabisha walinzi wake kumuondoa jukwaani kwa muda. Wafuasi wake wanasema walinzi wake walifanikiwa kumuondoa jukwaani licha ya hofu kwamba kulikuwa na mtu aliyekuwa amejihami kwa silaha miongoni mwao. Bw.Trump alikuwa anakaribia kilele cha hotuba yake ndani ya ukumbi wa Reno uliyojaa wafuasi wake, na ghafla kukatokea rabsha karibu na jukwaa. Taharuki ilitanda mahala hapo kabla ya walinzi wake kufanikiwa kumuondoa. Wafuasi wake waliyojawa na hofu walianza kukimbilia lango la kutoka nje wa ukumbi huo kufuatia madai ambayo hayakudhibitishwa Polisi wamemkamata mtu mmoja kufuatia tukio hilo lakini akaachiliwa muda mfupi baadaye. Mtu huyo hakupatikana na silaha kama ilivyodaiwa. Huku zikiwa zimesalia siku tatu kabla ya uchaguzi mkuu,wagombea wote wawili wameimarisha kampeini zao katika jimbo muhimu la Florida linalo na umaarufu w

Idadi ya wakimbizi raia wa Burundi wanaoendelea kuikimbia nchi yao kutokana na machafuko ya kisiasa yaliyoanza toka mwezi April mwaka jana nakupewa hifadhi katika kambi ya Nduta iliyopo wilayani Kibondo Mkoani Kigoma imeendelea kuongezeka siku hadi siku.

Idadi ya wakimbizi raia wa Burundi wanaoendelea kuikimbia nchi yao kutokana na machafuko ya kisiasa yaliyoanza toka mwezi April mwaka jana nakupewa hifadhi katika kambi ya Nduta iliyopo wilayani Kibondo Mkoani Kigoma imeendelea kuongezeka siku hadi siku. Hayo ya mebainishwa na mkuu msaidizi wa kambi hiyo Bi Jeska Ntaita alipozungumza na  Clouds fm kuhusiana na idadi ya wakimbizi wanaoendelea kupokelewa kwenye kambi hiyo pamoja na changamoto kwenye kambi hiyo. Amesema hadi sasa kambi hiyo imepokea zaidi ya wakimbizi 55,500 (hamsini natano elfu na miatano) na kwamba changamoto ya maji iliyokuwa ikiikabili kambi hiyo ikiwa inaendelea kushughulikiwa Aidha Bi Ntaita amesema kambi hiyo ilisimama kupokea wakimbizi hao kutokana na hapo awali kuwa natatizo kubwa la uhaba wa maji na sasatatizo la hilo la limeshughulikiwa na sasa wana mpango wakuendelea kuwapokea wakimbizi hao hadi kufikia 60,000 ilikupunguza msongamano kwenye kambi zingine zinazoendelea kuwapokea Baadhi ya wakimbi

Wakati jamii nyingi zikihangaika kuhakikisha watoto wao wanapata elimu kwa namna yoyote ile, hali imekuwa tofauti kwa baadhi ya wazazi wengine ambao wamewakikataa watoto wao kuendelea na elimu ya juu kwa madai wao ni masikini

Picha
Wakati jamii nyingi zikihangaika kuhakikisha watoto wao wanapata elimu kwa namna yoyote ile, hali imekuwa tofauti kwa baadhi ya wazazi wengine ambao wamewakikataa watoto wao kuendelea na elimu ya juu kwa madai wao ni masikini Amos Mabula ambae ni mwalimu mkuu wa shule ya Nyakasanda , iliyoko Tarafa ya Mabamba wilayani Kibondo Mkoa wa Kigoma,  alipokuwa akiongea na clouds Tv, amesema kutokana na mwamko mdogo wa elimu, miongoni mwa baadhi ya wazazi, wamekuwa wakiwazuia watoto kufanya vizuri kwenye mihani yao kuhitimu elimu ya msingi kwa kisingizio kuwa wakifaulu wao hawana uwezo wa kuwasomesha Amesema kutokana na hali hiyo baadhi ya wanafunzi wamekuwa wakichora picha za wanyama kwenye karatasi za kujibia mitihani japo majina yao uandikwa kwa usahii  Afisa elimu shule za msingi wilayani humo Joseph Tirutangwa, alipotembelea shule hiyo na kuongea  baadhi jamii amewataka kuachana na mawazo potofu kwani hali hiyo ni kuharibu maisha ya watoto wao Hata hivyo mmoja wa w

Kibondo;Wanafunzi wanaosoma katika shule binafsi wameeleza kukabiliwa na tatizo la walimu wanaopata ajira za muda katika shule zao na kisha kuondoka baada ya muda mfupi, kuwa hali hiyo inawahathiri kimasomo na kupelekea kushuka kwa kiwango cha elimu katika shule hizo tofauti na mategemeo yao

Picha
Lidia  ladislaus Mwanafunzi shule ya sekondari Bishop Mpango Baadhi ya wanafunzi shule ya sekondari Mt Thomas More Kibogora Jeremia Gwegenyeza makamu mwenyekiti  CHAMA CHA WAMILIKI WA SHULE BINFSI  WANAFUNZI SHULE YA SEKONDARI bISHOP mPANGO  Kibondo; Wanafunzi wanaosoma katika shule binafsi wameeleza  kukabiliwa na tatizo la walimu wanaopata ajira za muda katika shule zao na kisha kuondoka baada ya muda mfupi, kuwa hali hiyo inawahathiri kimasomo na kupelekea kushuka kwa kiwango cha elimu katika shule hizo tofauti na mategemeo yao Wakizungumza kwa nyakati tofauti baadhi ya wanafunzi hao, ambao ni Peter Lyoba kutoka shule ya sekondari Kibogora iliyoko wilayani Kakonko, na Lidia Shija shule ya Sekondari Bishop Mpango ya wilayani Kibondo Mkoani Kigoma wamesema  kwakuwa kila mwalimu ana namna yake ufundishaji , hivyo wanapobadirishiwa walimu kila mara uwasababishia usumbufu kuanza upya kumuelewa ‘’Wakuu wengi wa shule binafsi wanategemea

Kakonko;Naibu waziri Ofisi ya Rais serikali za mitaa Tawala za mikoa Tamisemi Seleman Jafo amewataka wakuu wa Idara za halmashauri za wilaya kuhakikisha wanashirikiana na wafanyakazi walio chini yao katika utendaji kazi ili kuleta tija na kuondoa kukata tamaa kwa wafanyakazi

Kakonko; Naibu waziri Ofisi ya Rais serikali za mitaa Tawala za mikoa Tamisemi Seleman Jafo amewataka wakuu wa Idara za halmashauri za wilaya kuhakikisha wanashirikiana na wafanyakazi walio chini yao katika utendaji kazi  ili kuleta tija na  kuondoa kukata  tamaa kwa wafanyakazi Wito huo aliutoa jana  alipokuwa akizungumza na Watumishi wa halmashauri ya wilaya ya Kakonko mkoani Kigoma katika ziara yake ya kutembelea baadhi ya mikoa na wilaya kukagua shuguli za maendeleo Jafo alisema kumekuwepo na baadhi ya wakuu wa idara ambao hawana mausiano mazuri na wafanyakazi wa nchini yao hali inayopelekea wengi kukata tamaa ya kazi na kufanya shuguli za maendeleo ya kuwahudumia wananchi kutokuwa na mafanikio ‘’Kitu cha kusikitisha ni pale mfanyakazi anapoka muda mrefu bila kupandaraja huku wanaojiriwa nyuma yake wanapanda kisa hajatoa rushwa na rushwa mbaya zilizopo ni rushwa za ngono jamani wakuu wa idara watendeeni watu mema maafisa utumishi jipangeni vizuri kwa kusimamia idara ze

Marekani na Urusi zimelaumiana vikali kwenye baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa juu ya mashambulizi dhidi ya msafara wa misaada nchini Syria, pamoja na hatua ya kuvunja mkataba wa kusitisha mapigano.

Picha
Moja ya malori yaliyoteketezwa Marekani na Urusi zimelaumiana vikali kwenye baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa juu ya mashambulizi dhidi ya msafara wa misaada nchini Syria, pamoja na hatua ya kuvunja mkataba wa kusitisha mapigano. Wamarekani wamekuwa wakiamini kuwa Urusi ndio iliyoshambulia msafara huo, huku Warusi wakilipinga hilo. Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Urusi John Kerry, alitoka nje ya lugha ya kidiplomasia kwa kutumia dhihaka zaidi. Huku mwenzake wa Urusi Sergey Lavrov akipinga hisia hizo kali kwa kuorodhesha mifano kadhaa kutetea nchi yake. Aidha ametaka pia kufanyika Licha ya majibizano makali, Urusi na Marekani zilikubaliana kwa pamoja kuongoza mkutano wa mataifa 23, yanayoiunga mkono Syria ambao utafanyika mjini New York, baadaye leo. Katika hatua nyingine Umoja wa Mataifa umesema unajiandaa kuanza tena kutoa misaada ya kibinadamu katika maeneo yaliyozingirwa nchini Syria, baada ya kusitishwa kwa usambazaji wa misaada kufuatia shambulio hilo. Mjumbe

Maafisa wa jeshi la ulinzi wa rais wamehusika katika shambulio dhidi ya makao makuu ya chama cha upinzani, watu wawili waliojeruhiwa wameambia BBC.

Picha
Add caption Maafisa wa jeshi la ulinzi wa rais wamehusika katika shambulio dhidi ya makao makuu ya chama cha upinzani, watu wawili waliojeruhiwa wameambia BBC. Makao makuu ya vyama vitatu vya upinzani katika Jamhuri ya kidemokrasi ya Congo yaliteketezwa moto katika mashambulio ya usiku kwenye mji mkuu Kinshasa. Kumekuwa na miili ya watu wawili ilioteketezwa moto katika ofisi hizo zilizoharibiwa za muungano mkuu wa upinzani DRC (UDPS). Msemaji wa jeshi la Congo ameiambia BBC hana la kusema kuhusu shutuma hizo. Upinzani unasema zaidi ya watu 50 wameuawa Jumatatu wakati wa maandamano kumpinga rais Joseph Kabila. Serikali inasema idadi ya waliouawa ni watu 17. Vikosi vya usalama vimeshutumiwa kwa kutumia risasi dhidi ya waandamanaj hao wa amani waliotaka kutolewa tarehe ya uchaguzi wa urais nchini.

Kakonko; Watanzania wametakiwa kujenga tabia ya kulinda mali za umma huku wakitambua kuwa ni kodi za na ni kwa manufaa yao wenyewe hivyo hawana budi kutoa taarifa katika mamlaka husika pale wanapoona kuna dalili za kuhodhiwa au kuhujumiwa kwa mali hizo

Picha
Baadhi ya wananchi na wafanyakazi wa halmashauri ta kakonko waliohudhiria utilianaji wa sahihi mkataba ujenzi wa halmashauri hiyo kati yake na kampuni Magaco ya mjini Dodoma Kakonko; Watanzania wametakiwa kujenga tabia ya kulinda mali za umma huku wakitambua kuwa  ni kodi za na ni kwa manufaa yao wenyewe hivyo hawana budi kutoa taarifa katika mamlaka husika pale wanapoona kuna dalili za kuhodhiwa au kuhujumiwa kwa mali hizo Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Kakonko mkoani Kigoma Lusubiro Joel akizungumza wakati wa hafla fupi ya kutiliana saini mkataba wa ujenzi wa ofisi za Halmashauri ya wilaya hiyo na Mkandarasi Magacon Constraction limited ya Mjini Dodoma juzi, Lusubiro alisema watu wengi ubaki wakilalamika  badala ya kutoa taarifa ili kuzuia uharibifu zaidi huku akiwasisitiza wananchi kutembelea eneo la ujenzi wa osifi hizo na kuhoji pale wasipoelewa mambo juu ya mambo yanayoendelea ‘’Tumeamua katika halmashauri yetu kufanya mambo wazi hale yale yanayotak

Madereva nane wa malori kutoka nchini Tanzania na wengine wanne kutoka Kenya wameokolewa baada ya kushikwa mateka mashariki mwa Jamhuri ya Demokrasi ya Congo

Picha
Madereva nane wa malori kutoka nchini Tanzania na wengine wanne kutoka Kenya wameokolewa baada ya kushikwa mateka mashariki mwa Jamhuri ya Demokrasi ya Congo. Madereva hao walitekwa nyara katika mkoa ulio kusini wa Kivu siku ya Jumatano. Wizara ya mashauri ya nchi za kigeni nchini Tanzania ilisema kuwa watekaji nyara wao walikuwa wakiitisha fidia ya dola 4,000 kwa kila dereva. Hata hivyo waziri wa masuala ya ndani nchini Congo Zakwani Salehe, alisema kuwa hakuna fidia iliyolipwa na ni wanajeshi waliowaokoa madereva hao Aliwataja watekaji hao kama majambazi na haijabainika ikiwa walikuwa na uhusiano na kundi lolote la waasi linaloendesha shughuli zake mashariki mwa Jamhuri ya Demokrasi ya Congo. Mwandishi wa BBC aliyeko mjini Bukavu anasema kuwa visa vya utekaji nyara kwa fidia vinazidi kuongezeka Malori hayo yalichomwa moto na madereva wake kutekwa nyara Mara nyingi bidhaa husafirishwa kwende DRC kutoka mataifa jirani kwa njia ya barabara

Umoja wa Mataifa unasema kuwa idadi ya watu waliokimbia nchi ya Sudan Kusini kutokana na vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini humo imepita watu milioni moja

Picha
Umoja wa Mataifa unasema kuwa idadi ya watu waliokimbia nchi ya Sudan Kusini kutokana na vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini humo imepita watu milioni moja. Idadi hiyo inajumuisha zaidi ya watu 185,000 ambao wameikimbia nchi kufuatia mapigano mapya yaliyoanza mwezi Julai. Zaidi ya watu milioni 1.6 nao wamelazimika kuhama makwao ndani ya Sudan Kusini. Kati ya hao wakimbizi 373,626 wameingia nchini Uganga huku theluthi moja kati yao wakiwasili tangu mwezi Julai na 20,000 wiki iliyopita. Wale wanaowasili sasa wanasema kuwa kuna mapigano mapya huku raia wakishambuliwa na makundi yaliyojihami ambayo hupora, huwadhulumu kimapenzi wanawake na wasichana na kuwaingiza jeshini vijana wa kiume. Wakimbizi 292,000 waliingia nchini Ethiopia huku 11,000 wakivuka na kungia Gambella wiki iliyopita. Wale wanaowsili kwa sasa wanatoka jamii ya Nuer wakiwemo watoto 500 wasioandana na wazazi. 247,317 wamewasili nchini Sudan, 1800 wakiwasili kila mwezi katika jimbo la White Nile na mafuriko yakiwa

Wanahabari nchini Kenya walaani dhuluma wanazofanyiwa

Picha
Waandishi wa habari nchini Kenya wameandamana Nairobi na miji mingine kupinga kile wanachosema ni kuongezeka kwa visa vya wanahabari kutishiwa na hata kuuawa. Maandamano yaliitishwa na Chama cha Waandishi wa habari ambacho kinasema wanahabari watano wamefariki katika hali ya kutatanisha katika kipindi cha mwaka mmoja. Maandamano yamefanyika siku kadhaa baada ya mwandishi wa habari za kisiasa kufariki katika mazingira ya kutatanisha eneo la Kilifi, pwani ya Kenya. Katika waraka wao walioutuma kwa bunge waandishi hao walilalamika kuhusu namna wanavyoshambaliwa na kupokea vitisho vya kuuawa kutoka kwa wanasiasa na umma. Wamesema baadhi ya viongozi wa kisiasa wa serikali kuu, kaunti pamoja na raia wamekuwa wakijiamulia wenyewe kuchukua sheria mkononi kuidhinisha mateso na kuwashambulia waandishi wa habari kwa kuwapiga na kuwatusi kwenye mitandao ya kijamii na baadhi yao kuwatishia mauaji ikiwa hawatatoa taarifa zinazowapendelea. Wamesisitiza kuwa wanayo haki ya kikatiba ya ku

Rais wa Marekani Barack Obama na kiongozi wa Ufilipino Rodrigo Duterte wamekutana ana kwa ana siku moja baada ya kiongozi huyo wa Ufilipino kuonekana kumtusi Bw Obama.

Picha
Jumanne, Bw Obama alifutilia mbali mkutano uliokuwa umepangwa kati ya wawili hao baada ya Bw Duterte kumuita "mwana wa kahaba". Walikutana kwa njia isiyo rasmi muda mfupi kabla ya dhifa ya jioni ya viongozi wa nchi za Kusini Mashariki mwa Asia nchini Laos. Msemaji wa serikali ya Ufilipino alisema alikuwa na furaha sana kwamba mkutano huo ulifanyika. Obama afuta mkutano na kiongozi wa Ufilipino Mfahamu rais Duterte, kiongozi aliyemtusi Obama Maafisa wa Marekani walisema ulikuwa "mkutano mfupi" kabla ya dhifa iliyoandaliwa viongozi katika eneo la "kuketi viongozi". Bw Obama na Bw Duterte wanadaiwa kuingia kwenye ukumbi wa dhifa nyakati tofauti na hawakuzungumza au kukaribiana wakati wa hafla hiyo iliyodumu saa moja na dakika 20. "Walikuwa wa mwisho kuondoka ukumbini. Siwezi kusema walikutana kwa muda gani," waziri wa mambo ya nje wa Ufilipino Perfecto Yasay, aliyesafiri na Bw Duterte, aliwaambia wanahabari baadaye. "Nina furah

Kibondo;Chuo cha Uuguzi kilichoko Wilayani Kibondo mkoani Kigoma kina kabiliwa na matatizo mbalimbali ikiwa ni pamoja na ukosefu wa miundo mbinu ya majengo fedha kwa ajili ya kuendeshea chuo hicho na ukosefu wa watumishi wakutosha hali inayopelekea kuathili ufundishaji

Picha
Alfrida Ndungulu mkuu wa chuo Atashasta Nditiye Mbunge jimbo la Muhambwe Kibondo; Chuo cha Uuguzi kilichoko Wilayani Kibondo mkoani Kigoma kina kabiliwa na matatizo mbalimbali ikiwa ni pamoja na ukosefu wa miundo mbinu ya majengo fedha kwa ajili ya kuendeshea chuo hicho na ukosefu wa watumishi  wakutosha hali inayopelekea kuathili ufundishaji Chuo hicho hakina Jengo la Maabara kwa ajili ya kujifunzia kwa vitendo kwa wanafunzi walimu waliopo ni watatu na mahitaji wanatakiwa wapo walimu kumi na tano Akiongelea swala hilo jana  katika mahafali ya saba  kwa wahitimu ngazi ya cheti mkuu wa chuo hicho Alfreda Ndungulu alisema licha ya walimu kujituma kufanya kazi kwa bidii lakini changamoto hizo zimekuwa zikiwalemea kwa kukosa mahitaji muhimu kama vifaa vya maabara kwa ajili ya kufundishia huku akiiomba serikali kupitia wizara ya Afya maendeleo ya Jamii Jinsia, Wazee na Watoto kulitazama kwa namna ya pekee Nao wanafunzi waliokuwa wakihitimu kwen

Kakonko;Vijana wanaomaliza mafunzo awali ya kijeshi katika vikosi vya jeshi la kujenga Taifai hapa nchini wametakiwa kuwa na unyenyekevu na nidham na kufuata taratibu na sheria za nchi wakizingatia mafunzo na maelekezo wanayopewa, ili jamii iweze kupata manufaa ya kuwepo kwa jeshi hilo

Picha
Mwemezi MuhingoMwananchi Kakonko; Vijana wanaomaliza mafunzo awali ya kijeshi katika vikosi vya jeshi la kujenga Taifai hapa nchini    wametakiwa kuwa na unyenyekevu na nidham na kufuata taratibu na sheria za nchi wakizingatia mafunzo na maelekezo wanayopewa, ili jamii iweze kupata manufaa ya kuwepo kwa jeshi hilo Akiwahutubia jana, mamia ya wahitimu wakufunzi , Askali na wananchi wa kawaida wakati wa kufunga mafunzo ya kijeshi kwa vijana mujibu wa sheria Oparation Magufuli Mkuu wa wilaya ya Kakonko Mkoani Kigoma Canol Hosea Ndagala ambae alikuwa mgeni rasmi kikisi 824 Kanembwa amesema kwa kuwa Askali ni Raia daraja la pili hivyo ni lazima kufuata maadili na kinyume chake huyo si Askali Mkuu wa JKT hapa nchini Brigedia General  Michael Isamuyo  aliyewakilishwa na Luten Canol Joseph P Mahende aliwambia wahitimu hao kuwa ni mambo mengi waliyojinfunza jeshini ambayo hapo awali hawakuyafahamu walipokuwa mashuleni, hivyo ni vema wakayazingatia kw