UKOSEFU WA WATAALAM WA MAZINGIRA VIJIJINI






 Kibondo.Ili kuweza kufanikisha mapambano ya mabadiliko ya Tabia nchi serikali imeshauri kuweka utaratibu wa uwepo  wataalam wa mazingira katika maeneo ya vijijini kama ilivyo kwa maafisa ugani ili watoe ushauri wa utunzaji wa mazingira


Hayo yalisemwa jana  na baadhi ya Wakazi wa Wilaya za Kakonko na Kibondo Mkoani Kigoma  ambao ni George Daniel na Joyce Alex walipokuwa kwenye mafunzo ya utunzaji wa Mazingira yaliyoandaliwa na Kanisa la Free Pentekoste Jimbo la Kibondo ambapo wamesema Wananchi wengi wanaoishi Vijijini wanashindwa kuendesha shuguli za upandaji Miti kutokana na kukosa uelewa

Wamesema kwa sasa kumekuwepo na mwitikio mkubwa wa Wananchi katika sualautunzaji wa mazingira hasa katika upandaji Miti lakini wamekuwa wakikosa uelewa  na kuharibikiwa katika Vitaru ya uoteshaji na Mashambani  hatua ambayo imekuwa ikipekea hali ya kukata tamaa

''Tunawaomba Wadau wa Mazingira na serikali kulitazama kwa umakini suala hili kwani miti imekuwa ikikatwa hovyo hivyo jitiada za upandaji wakitaalam ni wa lazima pamoja na hamasa ili kufikia malengo yanayokusudiwa''alisema George Mshiriki wa mafunzo

Kwa upande wake Mratibu wa Mradi wa Mazingira kupitia Jimbo hilo Leopod Muhagaze amesema katika kuhakikisha wanatimiza malengo    yao upandaji Miti, wamekuwa wakishirikiana na maafisa Mazingira ngazi  za  wilaya  Kakonko na Kibondo kuyaelemisha Makundi katika maeneo ya Vijijini japo hawakidhi haja

Katika hatua ya kukabiliana na changamoto ya ukosefu wa Wataalam wa Mazingira kwenye kata na Vijiji upo mpango wa kutoa elimu kwa Viongozi wa Vikundi ambao nao watawaelimisha wenzao Vijijini  namna ya upandaji Miti ulinzi wa vyanzo vya Maji pamoja na sheria na sera za utunzaji wa Mazingira

Aidha Leopod aliongeza kuwa licha ya Vikundi kuhamasihwa kutunza Mazingira wamekuwa wakipewa elimu ya kuinua uchumi wao kupitia Vikundi vya ujasriamali ambapo Wananchi wamekuwa wakipewa Mbegu na Vifaa vya kumwagilia Miche

Kanisa la FPCT Jimbo la Kibondo liliamua kuanzisha mradi wa Mazingi kwa waumini wake ili kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi ambayo yamekuwa yakipelekea kushuka uchumi lina lenga kuhumia Vikundi 100 na hadi sasa vipo vikundi 50  11 viko wilayani Kibondo na 39 viko wilaya ya Kakono na zimeshatumika Sh 17 milion kuanzi januari 2022 hadi sasa

Mpango huo ulifanikisha kupanda Miti  elfu kumi kwa mwaka 2022 kupitia Vikundi na Mtu mmoja mmoja katika maeneo ya Makazi kama anavyoeleza Askofu wa Kanisa Hilo Jimbo la Kibondo Enos Ntibalosiga huku akisistiza waumini wa Kanisa hilo kutambua umuhimu wa utunzaji wa Mazingira
Washiriki wakiwa kwenye Mafunzo ya utunzaji wa Mazingira

Leopod Muhagaze Mratibu Mradi wa Mazingira na Mkufunzi


george Daniel Mshiriki

Enos Ntibalosiga Askofu Kanisa  FPCT Jimbo la Kibondo



Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao