Magu yapunguza vifo vitokanavyo na uzazi asilimia 70 kwa miaka mitano
Mwanza. Wilaya ya Magu Mkoani Mwanza imefanikiwa kupunguza Vifo vitokanavyo na uzazi kutoka vifo 112 hadi 42 katika kipindi cha miaka mitano baada ya serikali kuboresha huduma kwa kutoa vifaa na kuongeza miundombinu ya majengo
![]() |
| Voronica Gibson Mkazi wa Magu |
![]() |
| Hellen Chizere Muuguzi mfawidhi Hospitali ya Wilaya ya Magu |
![]() |
| Raphaem Mhana Mganga Mkuu W ya Magu |
Raphael Mhana Mganga Mkuu Wilaya ya Magu Mkoani Mwanza ameeleza kipindi cha2015hadi 2020, hali ilikuwa hairidhishi ikilinganishwa na takwimu kuanzia 2020 hadi 2025 baada ya kufanyika maboresho katika sekta ya Afya
Hata hivyo Mhana amesema kutokana na maboresho hayo
kwa sasa wanatengeza na Miguu bandia ambayo inasaidia Watu wanaopata matatizo
mbalimbali zikiwemo ajali
‘’Wagonjwa wenye Matatizo ya Viungo hasa Miguu
walemavu wa kuzaliwa na wanaokuwa wamepata ajali katika Wilaya ya Magu na
maeneo ya jirani,wamekuwa wakisafiri kwenda mbali kutafuta huduma ya Miguu
bandia lakini kwa hivi sasa baada ya
Miguu bandia kuanza kutengenezwa hapa,usumbufu umepungu katika jamii zetu’’amesema
Mhana Mganga Mkuu Wilaya ya Magu
Kwa upande wake muuguzi mfawidhi wa hospitali ya
Wilaya hiyo , Hellen Chizere amesema awali hospitali ilikuwa na uwezo wa kulaza
wagonjwa 133 lakini kwa sasa wanalaza
Wagonjwa 176 huku baadhi ya wanawake waliopata pata huduma hospitalini hapo
ambao ni Veronika Gibson na Anna Johakimu wakazi wa Magu, wakieleza kuridhishwa
na huduma
‘’Mimi nilipokuwa nahitaji kujifungua nakufikishwa
katika Hospitali ya Wilaya nilihudumiwa Vizuri kwakuandaliwa na wauguzi na
Madaktari nikafanyiwa upasuaji nikiwa salma mimi na mwanangu, lakini
kilichonivutia ni vifaa ambavyo havikuwepo hapo nyuma maana hii ni mara ya tatu
kujifungua katika hospitali hii, maana huduma zinazopatikana kutokana na nyenzo
zinatia moyooamebainisha Anna Johakimu mmoja wa wanawake waliokuwa wamepata
huduma Hopitali ya wilaya ya Magu





Maoni
Chapisha Maoni