MANISPAA YA ILEMELA YAENDELEZA MPANGO WA UWEZESHAJI WANANCHI KIUCHUMI KWA KUTOA TSH 625 KWA ROBO YA TATU 2026 10% MAKUNDI MAALUM















 

Watu milioni 800 duniani wanatajwa kuishi katika umaskini uliokithiri na aina nyingi za umaskini zinasababishwa na kuongezeka kwa idadi ya watu wasio na ajira ajenda ya Umoja wa Mataifa ya Malengo ya Maendeleo Endelevu ya mwaka 2030, ambayo yameliweka suala la kupambana na umaskini kama lengo kuu kuzishauri nchi zote kuutokomeza umaskini

Kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa, siku ya kupambana na umaskini inaadhimishwa kwa kuzingatia wito uliotolewa miaka 25 iliyopita ya kutambua ujuzi na ujasiri wa familia zinazoishi katika umaskini duniani kote, umuhimu wa kuwafikia Watu maskini na kuwawezesha kiuchumi

Tanzania ni moja ya nchi Duniani ambayo inaendelea Mikakati ya kupambana na umasikini  kwa  kuwawezesha Wananchi kiuchumi ,kutokana na hatua hiyo, Manispaa ya Ilemela Mkoani Mwanza imeendeleza mpango huo ambapo katika robo ya tatu 2026 Vikundi 41 Vimepatiwa Mikopo ya 10%  amebainisha Kaimu Afisa Maendeleoa Manispaa hiyo Yusuph Okoko wakati wa hafla ya utoaji hudi

Ili kufikia malengo ya Serikalii walengwa wamehaswa kutumia vizuri Mikopo hiyo kwa kujituma katika kazi kwa weredi na kujali muda amewashauri Walengwa Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Amili Nkalipa

Fedha zilizotolewa kwa makundi ya Vijana Wanawake na Walemavu kwa roboya tatu ni Milion 625 Wanufaika ambao ni Laila Mkumbo na Jeni John  wakishukuru kwa hatua hiyo huku Mkuu wa Wilaya Amili Mkalipa akisistiza urejeshaji wa Mikopo kwa Wakati

‘’Mnapofanya kazi kumbukeni fedha hizo siyo msaada bali ni Mkopo hivyo lazima ulipwe na hatua zitachukuliwa kwa wale ambao hawatafanya utaratibu wa marejeshonasiyo vizuri tufike huko kwenye kusumbuana tena mnapolipa, mnatoa nafasi kwa wengine kukopa na nyie wenyewe najiongezea nafasi ya kukopa tena..alisema Nkalipa

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Shule ya msingi Nengo ya Walemavu, iliyoko wilayani Kibondo mkoani kigoma, inayohudumia wanafunzi walemavu wa mahitaji maalum inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwa ni ukosefu wa maji Vifaa vya kujinfunza na kufundishia na vyombo vya kulia chakula