RAIS SAMIA AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI SGR NA KUZINDUA MELI NNE ZA MIZIGO ZIWA TANGANYIKA

 










Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania







Alan Mvano Mbunge Jimbo la Kakonko

Simon Siro Mkuu wa Mkoa wa Kigoma

Makame Mbalawa Waziri wa Uchukuzi






Na Emmanueli Matinde,Kigoma

Kigoma.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amwesema serikali imeendelea na jitihada mbali mbali za kuimarisha miundombiu ya usafiri na usafirishaji nchini ikiwemo ujenzi wa Reli ya kisasa, uendelezaji wa bandari na ujenzi wa barabara na viwanja vya ndege.

Dkt. Samia amesema hayo leo mkoani Kigoma mara baada ya kuzindua meli nne za mizigo ndani ya Ziwa Tanganyika, na kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa Reli ya kisasa (SGR) Tabora – Kigoma, chenye urefu wa kilomita 506 kitakachojengwa kwa gharama ya Shilingi Trilioni 7.4.

Amesema yote hayo yanafanyika kwa lengo la kuifungua nchi kibiashara na kiuwekezaji, kupunguza gharama za usafiri na usafirishaji na kurahisisha biadhaa kuyafikia masoko ya ndani na ya nje ya nchi.

Kwa upande wake Waziri wa Uchukuzi Profesa Makame Mbarawa, amesema meli nne mpya zilizozinduliwa, zitafungua enzi mpya za usafirishaji wa majini katika Ziwa Tanganyika, zitaongeza wa usafirishaji wa mizigo, kuimarisha usalama wa safari, kupunguza gharama za usafirishaji na kuimarisha biashara kati ya Tanzania, Congo na Burundi.

Wakizungumza kwa niaba ya wananchi Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kusini Nuru Kashakali, na Mbunge wa Jimbo la Kakonko Alan Mvano, wamesema Reli ya SGR inakwenda kupanua wigo wa biashara baina ya watu wa mkoa wa Kigoma na wa nchi jirani za Burundi na Congo DRC.

‘’Kwakweli tunaishukuru Serikali kwa jitiada zake zakuhakikisha Mkoa wa Kigoma na maeneo mengine yanafunguka kwani imekuwa ni vigumu wafanyabiashara kufikia mafanikio kutokana na garama kubwa za usafirishaji wa bidha kati ya Congo Kinshasa na Burundi kwani yanayotumika ni Magari pekee ila usafiri wa Meli na Reli utakuwa mkombozi’’ amesema Mvano

 

 

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

KATIKA KUKABILIANA NA MAJANGA YA MOTO SERIKALI IMETOA GARI LENYE MTAMBO WA KUZIMIA MOTO KATIKA WILAYA YA KIBONDO