Viongozi wa Vijiji na Kata simamien na kutoa elimu umuhimu wa Lishe

 



















Kibondo.Viongozi wa Kata na Vijiji wamehaswakuendelea kuhamasisha umuhimu wa Lishe na mpangilio wa matumizi ya vyakula kwa Watoto na watu rika zote ukiwemouchangiaji wa chakula Mashuleni ili kupunguza udumavu na kuinua kiwango cha Elimu

Amebainishahayo Afisa Lishe Wilaya ya Kibondo Tumaini Muna wakati wa kujadili ripoti ya utekelezaji afua za Lishe kwa robo yanne 2025/26 ambapo ameeleza kuwa licha ya shule zote kutoa huduma ya Chakula,wapo baadhi ya Wazazi ambao hawachangii chakula kwaajili ya Watoto waojambo ambalo halikubaliki

Aidha Munna ameongeza kuwa ili kukabiliana na changamo ya udumavu,ni lazima afua za lishe zisimamiwe kikamilifukuanzia ngazi za familia huku akisistiza viongozi kusimamia kwa Vitendo mafunzo yanayotolewa katika maadhimisho ya siku ya Afya ya Lishe ya Kijiji

‘’Hatuwezi kufikia malengo pasipo kwenda pamoja hivyo hao wazazi ambao hawajitolei katika uchangiaji wa huduma ya chakula wanakwenda kinyume hivyo elimu na usimamizi ni muhimu kwani wanaopata shida ni Watoto maana Mtoto kushinda njaa kuanzia asubuhi hadi alasiri ni kumdhoofisha’’ amesema Muna

Mwenyekiti wa Kikao hicho ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Kibondo Kanal Aggrey Magwaza amesema uthabiti wa upatikanaji wa chakula mashuleni utasaidia kupunguza mdondoko kwa Wanafunzi na upatikanaji wa chakula utaongeza hamasa kwa Wanafunzi kupenda kuudhuria masomo

Nao wajumbe wa Kikao hicho wameahidi kuendelea kushirikiana kwa pamoja kuhamasisha upatikanaji wa chakula mashuleni

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

RAIS SAMIA AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI SGR NA KUZINDUA MELI NNE ZA MIZIGO ZIWA TANGANYIKA

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu