SIKU YA HOMA YA INI
Kila ifikapo julai 28 kila mwaka Dunia uadhimisha siku ya homa
kali ya Ini, lengo ikiwa ni kujenga uelewa kwenye jamii kuhusu tatizo hilo na
namna ya kujihami na ili kuepukana na hali hiyo
Homa ya Ini ni kuvimba kwa ini. Kitendo cha ini kuvimba ghafla ndio huitwa Homa kali ya Ini. Sababu
zinazofahamika zaidi za ini kuvimba ghafla ni maambukizi ya virusi vya homa ya
ini aina A na E na ni katika matukio machache sana virusi vya homa ya Ini B na
C. Aina fulani za dawa za matibabu ambazo zina sumu zinaweza pia kusababisha
homa Kali ya ini. Mara nyingi inaweza kupona bila hata madhara makubwa au
kuhitaji matibabu lakini katika matukio machache huweza kusababisha ini
kushindwa kufanya kazi na wakati mwingine kifo.
Na hizi ndizo dalili za homa kaliya Ini
Bila kujali visababishi, dalili za homa kali ya ini ni pamoja
na:
- Kutapika, kuhara au maumivu
ya tumbo
- Rangi ya manjano kwenye
macho na ngozi.
- Choo kilicho na rangi
mpauko.
Kwa kawaida, homa kali ya ini inaweza kupona bila hata madhara
ya hapo kwa hapo Katika baadhi ya wagonjwa, maambukizi ya homa kali ya ini aina
B au C yanaweza kusababisha maambukizi sugu na kusababisha kovu, ini kushindwa
kufanya kazi au hata saratani. Homa kali ya ini inakuwa mbaya zaidi kwa watu
wazima kuliko watoto. Watu wazima huonesha zaidi dalili za ugonjwa kuliko
watoto na madhara makubwa zaidi ya ugonjwa huo ni kwa watu wenye umri mkubwa.
Idadi kubwa ya watoto huwa hawaoneshi kabisa dalili na ni
wachache sana ambao Ngozi na macho hubadilika rangi na kuwa manjano. Inaweza
ikaisha haraka bila matibabu au huduma maalum, lakini kuna wakati inaweza
kusabaisha ini kushindwa kufanya kazi au kifo. Kunawa mikono kunaweza kuepusha
mtoto kuambukizwa homa ya ini aina A na E.
Iwapo una hofu ya kwamba mtoto wako ana dalili za homa kali ya
ini, tafadhali onana na daktari ili upate ushauri wa jinsi ya kumpatia mtoto
wako huduma anayohitaji
Changamoto kubwa ni jamii kutokuwa na tabia ya kupima afya
ambayo husaidia kujua hali ya kiafya ya Mtu na namna ya kudhibiti au kuzuia
Magonjwa, na wengi wakiogopa garama za
upimaji na hofu ya kujua hali walizonazo
Licha ya uwepo wa Dalili za Magonjwa mbalimbali ambazo uelezwa
na wataalam wa huduma za afya, Watu wengi upoteza muda kwa kutumia njia za
kienyeji kama dawa za mitishamba na Waganga wa kienyeji.

Maoni
Chapisha Maoni