POLISI KIGOMA WAADHIMISHA WIKI YA POLISI JAMII KWA KUCHANGIA DAMU

 
























KIBONDO.Jehi la Polisi Mkoa wa Kigoma katika kuadhimisha wiki ya Polisi jamii, limefanya uafi na kuchangia Damu katika hospitali ya Wilaya ya Kibondoili kusaidia kuokoa maisha ya Watu wanaohitaji huduma hiyo

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoma SACP Pilmoni Makungu akiongea na Waandishi wa habari wakati wa zoezi hilo, amesemalicha ya kupunguza uhitaji wa Damu katika vituo vya kutolea huduma za Afya,lengo kubwa ni kuonyesha ushiriki wa Jeshi  hilo katika masuala ya Kijamii

Aidha Makungu ameongeza kuwa katika Wiki hii,zinafanyika shughuli mbalimbali ikiwa ni pamoja na Michezo, Usafiri na kuchangia Damu ili kuokoa maisha ya wahitaji wa Damu

Naye Mganga mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya ya Kibondo Colnely Livin zoezi hilo linaonyesha namna Polisi linavyoshiriki katika utoaji wa huduma ndani ya Jamii

Jumla ya Unit 36 za Damu zimepatikana katika zoezi hilo la uchangiaji Damu huku Jeshi hilo likiitaka jamii kuendelea kudumisha amani ambapo Mganga mfawidhi wa hospitali hiyo Colnely Livin akeleza kuwa Damu hiyo itasaidia kupunguza  huitaji wa Damu katika Hospitali hiyo na kulipongeza Jeshi hilo kwa maono hayo ya kuchangia Damu

Kwa upande wao baadhi ya Wananchi Jonathani Ndahana na Melani Amoni pamoja na kulipongeza Jeshi hilo la Polisi kujitoa kushiriki katika kazi za kijamii katka maadhimisho ya Polisi ya Jamii ni vema lijenge tabia ya kushikiana na Wananchi bila kusubili Matukio

‘’Tunalipongeza Jeshi hili kwa hatua hiyo maana tumezoea kuwa wao wapo kwa ajiliya mambo ya ulinzi pekee kumbe hata ushiriki wa mambo mengine  unawahusu na hali hii inajenga umoja na wananchi hata katika kudhibiti uharifu’’amesema Amosi

 

 

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

RAIS SAMIA AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI SGR NA KUZINDUA MELI NNE ZA MIZIGO ZIWA TANGANYIKA

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu